Nyumbani


Waziri wa Nchi Ofisi ya Makamu wa Rais (Muungano na Mazingira) Mhe. Mhandisi Hamad Yusuf Masauni (kulia) akisikiliza maelezo katika Banda la NEMC alipotembelea Banda hilo katika Kongamano la Vijana lililofanyika katika  Ukumbi wa Maktaba ya Chuo Kikuu cha Dar es Salaam, Juni 2, 2026 lenye kauli mbiu "Ushiriki wa Vijana katika Kutekeleza Dira 2050: Usimamizi Endelevu wa Mazingira na Uhimilivu wa  Mabadiliko ya Tabianchi"


Elimu ya Mazingira ikitolewa katika banda la NEMC katika Kongamano la Vijana lililofanyika katika  Ukumbi wa Maktaba ya Chuo Kikuu cha Dar es Salaam, Juni 2, 2026 lenye kauli mbiu "Ushiriki wa Vijana katika Kutekeleza Dira 2050: Usimamizi Endelevu wa Mazingira na Uhimilivu wa  Mabadiliko ya Tabianchi"

NEMC YASHIRIKI KONGAMANO LA VIJANA KUJADILI USIMAMIZI ENDELEVU WA MAZINGIRA NA DIRA 2050

Baraza la Taifa la Hifadhi na Usimamizi wa Mazingira (NEMC) limeungana na wadau mbalimbali wa Mazingira kushiriki Kongamano la Vijana lililofanyika Juni 2, 2026 katika Ukumbi wa Maktaba wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam (UDSM), likiwa na kaulimbiu isemayo "Ushiriki wa Vijana katika Kutekeleza Dira 2050: Usimamizi Endelevu wa Mazingira na Uhimilivu wa Mabadiliko ya Tabianchi."

Akifungua kongamano hilo, Waziri wa Nchi, Ofisi ya Makamu wa Rais (Muungano na Mazingira), Mhe. Mhandisi Hamad Yusuf Masauni, amesisitiza umuhimu wa vijana kushiriki kikamilifu katika uhifadhi wa mazingira na kukabiliana na athari za mabadiliko ya tabianchi ili kuhakikisha maendeleo endelevu na utekelezaji wenye mafanikio wa Dira ya Taifa ya Maendeleo 2050.


Kupitia kongamano hilo, NEMC imepata fursa ya kutoa elimu ya mazingira kwa vijana, kuhamasisha matumizi endelevu ya rasilimali na kujadili nafasi ya vijana katika kuibua suluhisho bunifu za kukabiliana na changamoto za mazingira na mabadiliko ya tabianchi kwa maendeleo ya Taifa ya sasa na vizazi vijavyo.





Mhandisi Adrian Kayombo akifafanua jambo kwa Naibu Waziri Ofisi ya Makamu wa Rais (Muungano na Mazingira) Mhe. Reuben Kwagilwa alipozuru Banda la NEMC Maadhimisho ya Wiki ya Mazingira Duniani yanayofanyika katika viwanja vya JKCC Jijini Dodoma.

NAIBU WAZIRI, OFISI YA MAKAMU WA RAIS, MHE. REUBEN KWAGILWA AZURU BANDA LA NEMC MAONESHO KUELEKEA SIKU YA MAZINGIRA DUNIANI

Naibu Waziri Ofisi ya Makamu wa Rais Muungano na Mazingira Mhe. Reuben Kwagilwa (wa katikati kulia) azuru Banda la NEMC Maadhimisho ya wiki ya Mazingira Duniani, katika viwanja vya Jakaya Kikwete Convention Center (JKCC) Jijini Dodoma ambapo leo tarehe 1 Juni ndio ufunguzi wa maonesho hayo. Kushoto kwake ni Naibu Katibu Mkuu, Ofisi ya Makamu wa Rais, Balozi Baraka Luvanda.

Naibu Waziri, Ofisi ya Makamu wa Rais (Muungano na Mazingira) Mhe. Reuben Kwagilwa (katikati kulia) akisikiliza maelezo kutoka kwa Meneja wa Kanda ya Kati, Bw. Novatus Mushi alipozuru Banda la NEMC katika Wiki ya Maonesho kuelekea Maadhimisho ya Siku ya Mazingira Duniani, Juni 5 2026 yaliyofanyika katika viwanja vya Jakaya Kikwete jijini Dodoma.






MWENYEKITI WA BODI YA NEMC AZUNGUMZA NA WADAU WA MAZINGIRA, NEMC@40

Mwenyekiti wa Bodi ya NEMC, Mhandisi Mwanasha Tumbo akizungumza wakati wa Maadhimisho ya Miaka Arobaini (40) ya Baraza la Taifa la Hifadhi na Usimamizi wa Mazingira (NEMC) yaliyofanyika tarehe 29 Mei 2026 katika Ukumbi wa Mikutano wa Julius Nyerere (JNICC), Jijini Dar es Salaam.

Katika mazungumzo hayo, amesisitiza umuhimu wa ushirikiano wa wadau mbalimbali katika kulinda na kuhifadhi mazingira, akieleza kuwa mafanikio ya NEMC katika kipindi cha miaka 40 yamechangiwa kwa kiasi kikubwa na ushiriki wa serikali, sekta binafsi, taasisi na wananchi.

Aidha, ametoa wito wa kuendelea kuwekeza katika elimu ya mazingira, matumizi ya teknolojia na utekelezaji wa sheria ili kuhakikisha mazingira yanalindwa kwa manufaa ya kizazi cha sasa na vijavyo.









NEMC IMEADHIMISHA MIAKA 40 TANGU KUANZISHWA KWAKE MWAKA 1986

 Baraza la Taifa la Hifadhi na Usimamizi wa Mazingira (NEMC) Mei 29, 2026  limeadhimisha miaka arobaini (40) tangu kuanzishwa kwake mwaka 1986.

Maadhimisho hayo yamewakutanisha Viongozi mbalimbali wa ndani na nje ya Tanzania pamoja na wadau kutoka taasisi za umma na binafsi pamoja na mabalozi wa Mazingira ambayo yamekuwa jukwaa muhimu la kubadilishana uzoefu katika suala zima la Uhifadhi na Usimamizi wa Mazingira.

Akizungumza katika Maadhimisho hayo, Mkurugenzi Mkuu wa NEMC Dkt. Immaculate Sware Semesi alisema miaka arobaini (40) ya NEMC ni hatua mpya ya kutekeleza majukumu kwa nguvu mpya na ufanisi, amesema katika miaka yote hiyo Baraza limejufunza, limeimarika na lipo tayari kuendelea kulitumikia Taifa kwa weledi na uzalendo.






































NEMC YATAMBUA MCHANGO WA TFS KAMPENI YA UPANDAJI MITI NCHI NZIMA

Baraza la Taifa la Hifadhi na Usimamizi wa Mazingira (NEMC) limetambua mchango wa TFS katika zoezi Zima la kampeni ya upandaji miti 40,000 n...