Nyumbani

NEMC YATAMBUA USHIRIKIANO KATI YAKE NA JESHI LA POLISI

Yashiriki mahafali ya kumi ya programu za vyuo vya polisi

Baraza la Taifa la Hifadhi na Usimamizi wa Mazingira (NEMC) limetambua mchango wa jeshi la polisi ulionao katika Utekelezaji wa Sheria ya Mazingira hasa suala la ulinzi na usalama kwa maafisa wakati wa ukaguzi, kudhibiti ukaidi na kuhakikisha hatua za kisheria zinachukuliwa katika masuala ya Mazingira nchini.

Hayo yamedhihirika wakati wa mahafali ya kumi ya programu za vyuo vya polisi yaliyofanyika Januari 29, 2026 katika viwanja vya chuo cha taaluma ya polisi Jijini Dar es Salaam ambapo Mkurugenzi Mkuu wa NEMC Dkt.Immaculate Sware Semesi ameshiriki.

Ushiriki wake ni muhimu katika kutambua mchango ilionao wa kuimarisha utekelezaji wa Sheria za Mazingira nchini kwani uhalifu wa kimazingira kama kelele chafuzi, uharibifu wa mazingira na biashara haramu ya taka hudhibitiwa kwa ufanisi zaidi hali inayoongeza utii wa Sheria, kurahisisha uchunguzi na uwasilishaji wa kesi mahakamani.

DKT. SEMESI AKAGUA UTEKELEZAJI WA MRADI WA KUDHIBITI MATUMIZI YA ZEBAKI

Mkurugenzi Mkuu wa Baraza la Taifa la Hifadhi na Usimamizi wa Mazingira (NEMC), Dkt. Immaculate Sware Semesi, amefanya ziara ya kukagua utekelezaji wa Mradi wa Kudhibiti Matumizi ya Zebaki kwa Wachimbaji Wadogo wa Dhahabu (EHPMP) katika maeneo mbalimbali ya uchimbaji mdogo.

Katika ziara hiyo, alitembelea mwalo wa mfano wa matumizi salama ya dhahabu unaojengwa llindi, kata ya Mwime wilayani Kahama; kituo cha teknolojia mbadala ya zebaki kijijini Bumva, kata ya Segese, Halmashauri ya Msalala; pamoja na kituo cha elimu ya kudhibiti matumizi ya zebaki kinachojengwa katika Halmashauri ya Mji wa Geita.


Aidha, Dkt. Semesi alikutana na Katibu Tawala wa Mkoa wa Geita, Ndugu Mohamed J. Gombati, na kujadili changamoto za mazingira pamoja na umuhimu wa kuanzishwa kwa Ofisi mpya ya kikanda ya NEMC mkoani Geita inayohudumia mikoa ya Geita, Shinyanga na Kagera.

Dkt. Semesi pia alisisitiza ushirikiano wa dhati katika kuhakikisha shughuli za kiuchumi zinaendelezwa sambamba na ulinzi endelevu wa mazingira.










KAMATI YA KITAIFA INAYOSHAURI MASUALA YA UTAFITI WA MAZINGIRA (ERAC) YAKUTANA KUPITISHA RASIMU YA MWONGOZO WA TAFITI ZA KIMAZINGIRA NCHINI

Kamati ya Taifa ya Ushauri wa Tafiti za Mazingira (Environmental Research Adivisory Committee - ERAC) yakutana mkoani Morogoro kufanya mapitio na kupitisha Rasimu ya Mwongozo wa Tafiti za Mazingira (National Environmental  Research Agenda - NERA) kupitia kikao chake cha siku mbili tarehe 29 na 30, Januari 2026 katika ukumbi wa mikutano wa EDEMA.

Akizungumza Mkurugenzi wa Usimamizi na Tafiti za Mazingira (DERM) kutoka Baraza la Taifa la Hifadhi na Usimamizi wa Mazingira (NEMC), Dkt. Menan Jangu wakati wa ufunguzi kwa niaba ya Mkurugenzi Mkuu wa NEMC, amesema mazingira ni suala mtambuka hivyo Mwongozo huu wa Tafiti za Mazingira ni muhimu sana katika kupata taarifa sahihi ambazo zinasaidia katika kufanya maamuzi juu ya maendeleo endelevu nchini.

Dr. Menani alifafanua kuwa “Ustawi wa Maisha yetu ya kila siku,, Uchumi wetu na masuala mbalimbali ya kijamii yanategemea afya ya mazingira; hivyo utunzaji wa mazingira yanatoa uhakika wa afya ya jamii lakini pia maendeleo endelevu ya shughuli za kila siku.

Aidha, alifafanua kuwa ili kufikia malengo ya Dira ya Taifa ya 2050 ni lazima kuwa na miongozo sahihi wa Tafiti za Mazingira ambayo itapatikana kwa kushirikisha wadau mbalimbali.

“Dira inatekelezwa kwa kuwa na miongozo au nyenzo mbalimbali ikiwemo suala zima la utafiti wa mazingira kupitia Agenda ya mazingira."

Aidha, alifafanua kuwa kamati hii inaundwa na wataalam wabobevu kutoka katika Taasisi za Elimu ya Juu, Wizara, Idara za serikali, kutoka katika sekta binafsi na mashirika yasiyo ya serikali; hivyo ni matarajio Rasimu ya Agenda inayojadiliwa itakuwa na uzito wa kipekee na kuwa nyezo sahihi katika utekelezaji wa Dira 2050.

Akizungumza Meneja wa Tafiti za Mazingira ambaye pia ni Mratibu wa Agenda ya Taifa ya Tafiti za Mazingira, Dkt. Rose Mtui amesema Agenda hiyo inatarajiwa kutolewa mwaka huu 2026 na huwa inadumu kwa kipindi cha miaka mitano kabla ya kupitiwa upya kwa lengo la kuingiza mambo mapya yanayojitokeza au mabadiriko ya sera na sharia mbalimbali.

Alibainisha kuwa, Rasimu ya agenda hii imetengenezwa kwa kuzingatia mambo mengi ikiwemo masuala mapya kama vile Uchumi wa Blue, Mabadiliko ya tabia nchi, Tekinolojia mpya (AI), changamoto ya utupaji holela wa plastiki, Kelele na Mitetemo nk. Pia Rasimu ya agenda imezingatia mambo mbalimbali ya Kisera, Dira ya Taifa, ilani ya Uchaguzi nk. Aidha, alisema kuwa rasimu hii imepitia gazi mbalimbali ambapo wadau walipata fulsa ya kupitia agenda iliyopita (NERA 2017-2022) na kufanya tathmini ya utekelezaji wa Agenda hiyo na kuibua mambo mapya ambayo yanatakiwa kuwekewa vipaumbele.




NEMC, EWURA NA PAU ZAJADILI UWEKAJI WA MIFUMO YA UDHIBITI HEWA CHAFUZI KATIKA MRADI WA EACOP

Baraza la Taifa la Hifadhi na Usimamizi wa Mazingira (NEMC) kwa kushirikiana na Mamlaka ya Udhibiti wa Huduma za Nishati na Maji Tanzania (EWURA) na Mamlaka ya Usimamizi wa Petroli Uganda (PAU) limefanya majadiliano ya kitaalamu na wataalam kutoka Mradi wa Kusafirisha Mafuta Ghafi kutoka Hoima, Uganda hadi Chongoleani, Tanga (EACOP) yaliyojikita katika usimikaji wa mifumo ya kudhibiti uchafuzi wa hewa inayosaidia kukusanya mvuke (Vapour Recovery Units – VRU) na hewa chafuzi zinazotokana na shughuli za usafirishaji, upakuaji na upakiaji wa mafuta.

Mifumo hiyo inalenga kulinda mazingira na afya za jamii zinazozunguka vituo mbalimbali vinavyotarajiwa kuwa na uzalishaji mkubwa wa gesi ya methane na gesi nyinginezo ndani ya mradi huo. 

Hatua hii ni sehemu ya juhudi za Baraza katika kuhakikisha kuwa miradi ya kimkakati inazingatia viwango vya ubora wa mazingira, hivyo kuchangia katika kulinda mazingira kwa maendeleo endelevu.







KATIBU MKUU DR. RICHARD MUYUNGI AKUTANA NA MENEJIMENTI YA NEMC

Katibu Mkuu, Ofisi ya Makamu wa Rais (Muungano na Mazingira) Dkt. Richard Muyungi amefanya ziara ya kikazi katika Ofisi za Baraza la Taifa la Hifadhi na Usimamizi wa Mazingira (NEMC), ambapo amekutana na Menejimenti ya Baraza kwa lengo la kujitambulisha na kujionea utekelezaji wa majukumu ya taasisi hiyo.



Katika kikao kilichohusisha pia Mameneja wa Kanda 13 nchi nzima kiliwasilisha taarifa za utekelezaji wa majukumu ya Baraza, ikiwemo mafanikio yaliyofikiwa, changamoto za mazingira zinazojitokeza pamoja na hali ya mazingira kwa ujumla. 

Aidha, ziliainishwa pia fursa za kiuchumi zilizopo katika sekta ya mazingira  hususani eneo la urejelezaji wa taka zinazoweza kuvutia uwekezaji na kuchangia maendeleo ya kiuchumi na uhifadhi endelevu wa mazingira.

Dkt. Richard Muyungi alipozungumza  ameishukuru NEMC kwa kazi kubwa wanayoifanya katika kuhifadhi na kusimamia mazingira ikiwa ni pamoja na kusimamia utekelezaji wa Sheria

Amesisitiza umuhimu wa Baraza  kuzingatia mabadiliko ya sayansi, teknolojia na mahitaji ya sasa ya jamii ili kuendana na ulimwengu wa kidigitali katika kufikisha elimu ya  Mazingira kwa jamii.

Katika maelekezo yake, Dkt. Muyungi ameitaka NEMC kuanzisha kitengo cha Ubunifu  kitakachokuwa na jukumu la kubuni na kuibua mawazo mapya yatakayosaidia kusukuma mbele gurudumu la maendeleo ya mazingira, ikiwemo kutatua changamoto zinazojitokeza kwa njia bunifu na endelevu.

Vilevile amesisitiza kuzingatiwa kwa weledi katika uchakataji na usimamizi wa miradi ili kuhakikisha miradi yote ya maendeleo inatekelezwa kwa kuzingatia Sheria, Kanuni na misingi ya uhifadhi wa mazingira.

Sambamba na hilo, aliagiza kuimarishwa kwa matumizi ya teknolojia ya kisasa itakayowezesha upatikanaji wa taarifa sahihi na za haraka za mazingira, jambo litakalosaidia katika kufanya maamuzi yenye tija na kulinda rasilimali za taifa.

Ziara hiyo ni ya kwanza kwa Dkt. Muyungi kufika na kuzungumza na Menejimenti ya NEMC tangu kuteuliwa kwake kushika wadhifa wa Katibu Mkuu Ofisi ya Makamu wa Rais (Muungano na Mazingira) na imeelezwa kuwa ni hatua muhimu katika kuimarisha ushirikiano, mawasiliano na uratibu wa masuala ya mazingira nchini.

NEMC YAUNGA MKONO JITIHADA ZA MHESHIMIWA RAIS DKT. SAMIA SULUHU HASSAN KATIKA KUTUNZA MAZINGIRA

Baraza la Taifa la Hifadhi na Usimamizi wa Mazingira (NEMC) limeunga mkono jitihada za Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan, za kuhifadhi na kusimamia mazingira kwa kushiriki zoezi la upandaji miti katika kuadhimisha siku yake ya kuzaliwa tarehe 27 Januari.
Katika kuadhimisha siku hiyo, Mheshimiwa Rais alipanda mti kama ishara ya kuhamasisha uhifadhi wa mazingira, ikiwa ni utekelezaji wa kaulimbiu isemayo “Uzalendo ni kutunza mazingira, shiriki kupanda miti.”
Kupitia kanda zake 13 nchini kote, NEMC imeshirikiana na wizara, taasisi za umma na binafsi, asasi za kiraia pamoja na kamati za mazingira kushiriki katika zoezi la upandaji miti katika maeneo mbalimbali yakiwemo shuleni, zahanati na katika masoko.


Akizungumza katika hafla hiyo, kwa niaba ya Mkurugenzi Mkuu, Mkurugenzi wa  Utawala na Fedha Bw. Dickson Mjinja alieleza umuhimu wa kupanda miti kama njia mojawapo ya kukabiliana na athari za mabadiliko ya tabianchi huku akisisitiza kuwa miti ina mchango mkubwa katika kuhifadhi ikolojia na kuboresha maisha ya binadamu.
Kwa upande wake, Meneja wa NEMC Kanda ya Ilala, Bi. Abella Muyungi, aliwataka wananchi kushiriki kikamilifu katika kusimamia na kuhifadhi mazingira nchini kwa vitendo, akisisitiza kuwa jukumu la uhifadhi wa mazingira ni la kila mmoja.

NEMC imeendelea kusisitiza dhamira yake ya kushirikiana na wadau mbalimbali katika kuunga mkono juhudi za Serikali za awamu ya sita chini ya uongozi wa Mheshimiwa Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan katika kulinda na kuhifadhi mazingira kwa maendeleo endelevu ya Taifa.

Zoezi la upandaji miti Kata ya Ilala viwanja vya msikate tamaa limeratibiwa na NEMC na Balozi wa Mazingira kutoka Ofisi ya Makamu wa Rais Bw. Grit Godfrey.



Akifafanua katika kikao hicho, Meneja wa Kanda ya Ilala, Bi. Abella Muyungi, alisema kuwa NEMC itaendelea kushirikiana kwa karibu na jamii na wadau wa mazingira katika kusikiliza na kushughulikia malalamiko ya mazingira, huku akisisitiza umuhimu wa wananchi kuzingatia sheria, taratibu na kanuni za mazingira kwa ajili ya kulinda afya ya binadamu na mazingira kwa ujumla.

Kupitia kikao hicho, NEMC ilisisitiza umuhimu wa ushirikiano kati ya jamii na wadau wa mazingira katika kulinda na kusimamia mazingira kwa maendeleo endelevu, huku ikiahidi kuendelea kutoa elimu na kuchukua hatua stahiki kwa mujibu wa sheria ili kuhakikisha mazingira yanahifadhiwa kwa manufaa ya kizazi cha sasa na kijacho. 








Mwenyekiti wa Bodi ya NEMC Mhandisi Mwanasha Tumbo akipanda mti, kuadhimisha siku ya kuzaliwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe.Dkt.Samia Suluhu Hassan

 "Uzalendo ni kutunza mazingira, shiriki kupanda miti "





NEMC YATAMBUA USHIRIKIANO KATI YAKE NA JESHI LA POLISI

Yashiriki mahafali ya kumi ya programu za vyuo vya polisi Baraza la Taifa la Hifadhi na Usimamizi wa Mazingira (NEMC) limetambua mchango wa ...