Nyumbani

NEMC YASHIRIKI KILELE CHA MAADHIMISHO YA SIKU YA MAZINGIRA DUNIANI-DODOMA

Baraza la Taifa la Hifadhi na Usimamizi wa Mazingira (NEMC) limeshiriki kikamilifu kilele cha Maadhimisho ya Siku ya Mazingira Duniani yaliyofanyika tarehe 5 Juni 2026 katika Ukumbi wa Mikutano wa Jakaya Kikwete (JKCC) Jijini Dodoma.

Maadhimisho hayo, yanayofanyika kila mwaka tarehe 5 Juni, kwa mwaka huu yaliadhimishwa kitaifa kwa kauli mbiu isemayo “Dira 2050: Tuwajibike Kukijanisha Tanzania”.


Mgeni rasmi wa hafla hiyo alikuwa Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Emmanuel Nchimbi ambapo kabla ya kilele cha Maadhimisho hayo kikitanguliwa na maonesho ya wiki nzima yaliyolenga kutoa elimu kwa wadau mbalimbali kuhusu uhifadhi na usimamizi wa mazingira kupitia banda lake maalum.

Katika hafla hiyo pia ulizinduliwa Mkakati wa Kitaifa wa Kukijanisha Tanzania ikiwa ni hatua kufikia Taifa linalostawi kiuchumi bila kuharibu Mazingira.

















NEMC YAMTAMBUA JACKLINE ELIABI KWA WASILISHO BORA LA UCHUMI MZUNGUKO KATIKA KILELE CHA MAADHIMISHO YA SIKU YA MAZINGIRA DUNIANI

Baraza la Taifa la Hifadhi na Usimamizi wa Mazingira (NEMC) limemtambua mwanafunzi wa Darasa la Sita, Jackline Eliabi wa Shule ya Msingi Manyinga, Wilaya ya Mvomero mkoani Morogoro, kwa uwasilishaji wake bora wa dhana ya Uchumi Mzunguko katika kilele cha Maadhimisho ya Siku ya Mazingira Duniani.

Jackline alipata pongezi na kutunukiwa zawadi baada ya kuwasilisha kwa umahiri dhana hiyo muhimu inayohamasisha matumizi endelevu ya rasilimali, upunguzaji wa taka na uhifadhi wa mazingira. Uwasilishaji wake ulionesha uelewa mkubwa wa masuala ya mazingira na mchango wa wanafunzi katika kuelimisha jamii kuhusu umuhimu wa kutunza mazingira kwa maendeleo endelevu.

Zawadi hiyo ilitolewa na Mkurugenzi Mkuu wa NEMC, Dkt. Immaculate Sware Semesi, ikiwa ni kutambua mchango wa wanafunzi katika kusukuma gurudumu la uhifadhi na usimamizi wa mazingira nchini. Dkt. Semesi alieleza kuwa wanafunzi ni wadau muhimu katika juhudi za kulinda mazingira na kwamba wao ndio mabalozi wa baadaye wa mazingira watakaosaidia kuendeleza agenda ya maendeleo endelevu kwa manufaa ya taifa na vizazi vijavyo.





DKT. NCHIMBI AZURU BANDA LA NEMC MAADHIMISHO YA SIKU YA MAZINGIRA DUNIANI

Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe.Dkt. Emmanuel Nchimbi ametembelea Banda la NEMC Leo ikiwa ni  siku ya kilele cha Maadhimisho ya Siku ya Mazingira Duniani yanayoadhimishwa kila tarehe 5, Mei ya Kila mwaka ambapo alipata fursa ya kujionea shughuli mbalimbali zinazotekelezwa na Baraza la Taifa la Hifadhi na Usimamizi wa Mazingira (NEMC) katika kuhifadhi na kusimamia mazingira nchini.


Maadhimisho ya mwaka huu yamefanyika chini ya kaulimbiu isemayo “Dira 2050: Tuwajibike Kukijanisha Tanzania,” ikihamasisha ushiriki wa wadau wote katika kutunza mazingira, kupambana na uharibifu wa mazingira na kuendeleza matumizi endelevu ya rasilimali asilia kwa maendeleo ya Taifa na ustawi wa vizazi vijavyo.





Waziri wa nchi Ofisi ya Makamu wa Rais (Muungano na Mazingira) Mhe. Mhandisi Hamad Yusuf Masauni (kushoto ) akipokea zawadi kutoka kwa Meneja wa Kanda ya Kati (NEMC) Bw. Novatus Mushi, mara baada ya kuzuru Banda la NEMC katika wiki ya Maonesho ya kuelekea Siku ya Mazingira Duniani  yanayofanyika viwanja vya  Jakaya Kikwete Convention Centre jijini Dodoma. Kilele cha Maadhimisho hayo ni tarehe 5 Juni 2026.

𝗠𝗪𝗘𝗡𝗬𝗘𝗞𝗜𝗧𝗜 𝗪𝗔 𝗕𝗢𝗗𝗜 𝗬𝗔 𝗡𝗘𝗠𝗖 𝗔𝗞𝗜𝗠𝗕𝗜𝗔 𝗞𝗜𝗟𝗢𝗠𝗜𝗧𝗔 𝟱

Mwenyekiti wa Bodi ya Baraza la Taifa la Hifadhi na Usimamizi wa Mazingira (NEMC), Mhandisi Mwanasha Tumbo, ameshiriki mbio za kilomita 5 zilizofanyika katika maadhimisho ya Siku ya Mazingira Duniani. 


Mbio hizo zililenga kuhamasisha jamii kuhusu umuhimu wa uhifadhi wa mazingira na kuendeleza afya kupitia shughuli za michezo.

Tukio hilo liliwakutanisha viongozi wa Serikali, wadau wa mazingira na wananchi mbalimbali, likibeba ujumbe wa pamoja wa kulinda mazingira kwa maendeleo endelevu na ustawi wa vizazi vya sasa na vijavyo.



WAZIRI MASAUNI AZURU BANDA LA NEMC MAONESHO WIKI YA KUELEKEA SIKU YA MAZINGIRA DUNIANI

Waziri wa nchi Ofisi ya Makamu wa Rais (Muungano na Mazingira) Mhandisi Hamad Yusuf Masauni azuru Banda la NEMC wiki ya Maonesho ya kuelekea Siku ya Mazingira Duniani  yanayofanyika viwanja vya  Jakaya Kikwete Convention Centre jijini Dodoma. Maonesho hayo yalifunguliwa rasmi tarehe 1 Juni 2026 ambapo kilele cha Maadhimisho hayo ni tarehe 5 Juni 2026 huku yakibeba Kaulimbiu "Dira 2050 - Tuwajibike Kukijanisha Tanzania"




𝗨𝗦𝗜𝗠𝗔𝗠𝗜𝗭𝗜 𝗪𝗔 𝗠𝗔𝗭𝗜𝗡𝗚𝗜𝗥𝗔 𝗨𝗘𝗡𝗗𝗘 𝗦𝗔𝗠𝗕𝗔𝗠𝗕𝗔 𝗡𝗔 𝗨𝗞𝗨𝗔𝗝𝗜 𝗪𝗔 𝗨𝗪𝗘𝗞𝗘𝗭𝗔𝗝𝗜 𝗡𝗪-𝗠𝗔𝗝𝗜, 𝗠𝗛𝗔𝗡𝗗𝗜𝗦𝗜 𝗞𝗨𝗡𝗗𝗢 𝗠𝗔𝗧𝗛𝗘𝗪

Naibu Waziri wa Maji Mhe. Mhandisi Kundo Andrew Mathew amesisitiza umuhimu wa NEMC kuharakisha mifumo ya mawasiliano na tehama katika kuratibu shughuli za Tathmini ya Athari kwa Mazingira na Jamii (TAM) na TISEZA kwenye upangaji wa maeneo ya uwekezaji na kuwataka kuwa na mpango kazi ulio wazi (clear roadmap) utakaoruhusu Tathmini za Athari kwa Mazingira na Jamii (TAM) kufanyika kwa haraka na ufanisi mkubwa, hatua itakayosaidia kuondoa urasimu na kuchochea kasi ya wawekezaji kuleta mitaji yao nchini.

Naibu Waziri wa Maji, Mhandisi Kundo Andrea Mathew, ameipongeza Baraza la Taifa la Hifadhi na Usimamizi wa Mazingira (NEMC) kwa ubunifu na mikakati thabiti wakati alipotembelea banda lao katika Maonesho ya Kuelekea Siku ya Mazingira Duniani.



NEMC YASHIRIKI KILELE CHA MAADHIMISHO YA SIKU YA MAZINGIRA DUNIANI-DODOMA

Baraza la Taifa la Hifadhi na Usimamizi wa Mazingira (NEMC) limeshiriki kikamilifu kilele cha Maadhimisho ya Siku ya Mazingira Duniani yaliy...