Nyumbani

NEMC YASHIRIKI KIKAMILIFU KONGAMANO LA ANWANI ZA MAKAZI NA MAONESHO YA TEKNOLOJIA ZA POSTA 2026

Baraza la Taifa la Hifadhi na Usimamizi wa Mazingira (NEMC) limeshiriki kikamilifu Kongamano la Mwaka la Anwani za Makazi na Maonesho ya Huduma za Posta kwa kutoa elimu ya Mazingira kwa wadau walioshiriki katika Kongamano hilo.

Kongamano hilo limehitishwa rasmi leo Februari 8, 2026 na Mgeni Rasmi Waziri wa Mawasiliano na Teknolojia ya Habari Mhe. Angellah Jasmine Mbelwa Kairuki (Mb) ambapo ameeleza umuhimu wa matumizi ya mfumo wa Anwani za Makazi (NAPA) na kusisitiza matumizi ya mfumo huo ili kuwezesha utambuzi wa makazi na Maeneo ambayo shughuli za kiuchumi zinazohitaji ufuatililiaji zinafanyika.

Kongamano hilo  lililobeba kauli mbiu isemayo "𝘼𝙣𝙬𝙖𝙣𝙞 𝙈𝙖𝙝𝙞𝙧𝙞 𝙣𝙖 𝙐𝙗𝙪𝙣𝙞𝙛𝙪 𝙬𝙖 𝙃𝙪𝙙𝙪𝙢𝙖 𝙯𝙖 𝙋𝙤𝙨𝙩𝙖 𝙠𝙬𝙖 𝙐𝙠𝙪𝙖𝙟𝙞 𝙅𝙪𝙢𝙪𝙞𝙨𝙝𝙞" lilianza Februari 5 na kuhitimishwa rasmi leo Februari 8, 2026 ambapo Kongamano hilo limefanyika kuanzia Februari katika Ukumbi wa  wa Kimataifa wa Julius Nyerere (JNICC) Jijini Dar es salaam.





𝗠𝗔𝗧𝗨𝗞𝗜𝗢 𝗞𝗔𝗧𝗜𝗞𝗔 𝗣𝗜𝗖𝗛𝗔-𝗞𝗢𝗡𝗚𝗔𝗠𝗔𝗡𝗢 𝗟𝗔 𝗠𝗪𝗔𝗞𝗔 𝗟𝗔 𝗔𝗡𝗪𝗔𝗡𝗜 𝗭𝗔 𝗠𝗔𝗞𝗔𝗭𝗜 𝗡𝗔 𝗠𝗔𝗢𝗡𝗘𝗦𝗛𝗢 𝗬𝗔 𝗧𝗘𝗞𝗡𝗢𝗟𝗢𝗝𝗜𝗔 𝗬𝗔 𝗛𝗨𝗗𝗨𝗠𝗔 𝗭𝗔 𝗣𝗢𝗦𝗧𝗔 𝟮𝟬𝟮𝟲

Elimu ya Mazingira ikiendelea kutolewa kwa wadau waliotembelea banda la NEMC katika Kongamano la Mwaka la Anwani za Makazi na Maonesho ya Teknolojia ya Huduma za Posta 2026 linalofanyika katika Ukumbi wa Mikutano wa Kimataifa wa Julius Nyerere (JNICC) Jijini Dar es salaam.

Maonesho hayo yenye kauli mbiu isemayo "𝘼𝙣𝙬𝙖𝙣𝙞 𝙈𝙖𝙝𝙞𝙧𝙞 𝙣𝙖 𝙐𝙗𝙪𝙣𝙞𝙛𝙪 𝙬𝙖 𝙃𝙪𝙙𝙪𝙢𝙖 𝙯𝙖 𝙋𝙤𝙨𝙩𝙖 𝙠𝙬𝙖 𝙐𝙠𝙪𝙖𝙟𝙞 𝙅𝙪𝙢𝙪𝙞𝙨𝙝𝙞" yanatarajiwa kuhitimishwa rasmi Februari 8, 2026.










NEMC YAUNGURUMA JNICC KONGAMANO LA ANWANI ZA MAKAZI

Yatoa Elimu ya Uhifadhi na Usimamizi wa Mazingira 

Baraza la Taifa la Hifadhi na Usimamizi wa Mazingira (NEMC) limetoa elimu ya mazingira kwenye Kongamano la Mwaka la Anwani za Makazi na Maonesho ya Teknolojia ya Huduma za Posta 2026 ihusuyo masuala mazima ya uhifadhi na usimamizi wa mazingira kwa mujibu wa Sheria ya Mazingira ya Mwaka 2004 na Kanuni zake katika  Kituo cha Kimataifa cha Mikutano cha Julius Nyerere (JNICC), jijini Dar es Salaam.

Akizungumza katika kongamano hilo linalotarajiwa kuhitimishwa Februari 08, 2026, Mhandisi Mkuu wa NEMC Bw. Jampyon Mbugi amesema kuwa matumizi sahihi ya anwani za makazi ni nyenzo muhimu katika kuimarisha usimamizi wa mazingira kupitia mfumo wa NAPA ambao utaiwezesha NEMC kupata taarifa muhimu za uhifadhi na usimamizi wa mazingira.

Ameongeza kuwa elimu hiyo inalenga kuwajengea wananchi uelewa wa majukumu yao ya kisheria na kijamii katika kulinda mazingira. Hata hivyo, anwani za makazi si utambulisho pekee wa maeneo bali ni chombo muhimu cha kupanga makazi na kusimamia mazingira kwa maendeleo yanayozingatia ustawi wa jamii na mazingira kwa ujumla. 

Naye Mhandisi Migodi NEMC, Bw. Hezron Mwashibanda ameeleza kuwa huduma zinazotolewa katika banda la NEMC ni pamoja na udhibiti wa kelele chafuzi, ufuatiliaji wa utekelezaji wa Tathmini ya Athari kwa Mazingira (TAM/EIA), pamoja na utekelezaji wa Sheria, ada za mazingira katika maeneo ya makazi na biashara.

NEMC inawakaribisha wananchi na wadau wote wa mazingira kupata elimu ya uhifadhi na usimamizi wa mazingira.



NEMC YASHIRIKI MAFUNZO YA REMOTE SENSING NA GIS

 Baraza la Taifa la Hifadhi na Usimamizi wa Mazingira (NEMC) limeshiriki katika mafunzo ya matumizi ya teknolojia ya Remote Sensing na Geographic Information Systems (GIS) yanayolenga kuimarisha uwezo wa taasisi za Serikali katika usimamizi, ufuatiliaji na uhifadhi wa rasilimali za bahari na uvuvi yanayofanyika kwa muda wa siku nne kuanzia Februari 3 hadi 6, 2026, jijini Dar es Salaam. 

Mafunzo hayo yameratibiwa na Korean Institute of Ocean Science and Technology (KIOST) kwa kushirikiana na Taasisi ya Utafiti wa Uvuvi Tanzania (TAFIRI) huku wadau zaidi ya 20 kutoka sekta ya Bahari na Uvuvi wanaotoka katika taasisi mbalimbali za Serikali zimeshiriki mafunzo hayo ikiwa ni pamoja na Baraza la Taifa la Hifadhi na Usimamizi wa Mazingira (NEMC), Taasisi ya Utafiti wa Uvuvi Tanzania (TAFIRI), Taasisi ya Utafiti wa Uvuvi Zanzibar (ZAFIRI), Dar es Salaam Maritime Institute (DMI), Chuo Kikuu cha Dar es Salaam (UDSM), Fisheries Education and Training Agency (FETA), Mamlaka ya Hali ya Hewa Tanzania (TMA), Deep Sea Fishing Authority (DSFA), pamoja na Wizara ya Mifugo na Uvuvi (MLF).

Aidha, Mafunzo haya ni sehemu ya jitihada za kuimarisha matumizi ya teknolojia ya satelaiti katika ukusanyaji na uchambuzi wa taarifa zitakazosaidia katika usimamizi endelevu wa rasilimali za bahari na uvuvi, pamoja na kukabiliana na athari za mabadiliko ya tabianchi.






NEMC KANDA YA ILALA YAKUTANA NA UONGOZI WA BENKI YA EQUITY KUJADILI FURSA ZA MAZINGIRA

 

NEMC Kanda ya Ilala, imekutana na uongozi wa Benki ya Equity kwa lengo la kujadili fursa za mashirikiano zilizopo katika sekta ya mazingira pamoja na utoaji wa elimu ya fedha. 

Kikao hicho kilichofanyika Januari 04, 2026 katika ofisi za NEMC jijini Dar es Salaam, kimeongozwa na Kaimu Meneja wa NEMC Kanda ya Ilala, Bi. Abela Muyungi, na kuwahusisha Meneja wa Tawi la Equity–Nyerere Road pamoja na Meneja wa Mahusiano wa benki hiyo. Majadiliano hayo yamejikita katika utoaji wa elimu ya mazingira, matumizi ya nishati safi, uzingatiaji wa sheria na kanuni za mazingira katika viwanda, pamoja na huduma za kifedha.




DKT. SEMESI ARIDHISHWA NA UTEKELEZAJI WA MRADI WA KUDHIBITI MATUMIZI YA ZEBAKI KWA WACHIMBAJI WADOGO WA DHAHABU (EHPMP)

Mkurugenzi Mkuu wa Baraza la Taifa la Hifadhi na Usimamizi wa Mazingira (NEMC) Dkt. Immaculate Sware Semesi ameonesha kuridhishwa na mambo mazuri yanayofanywa kupitia Mradi wa Kudhibiti Matumizi ya Zebaki kwa Wachimbaji Wadogo wa Dhahabu (EHPMP).

Dkt. Semesi ameonesha kuridhishwa huko Februari 2,2026 jijini Dodoma alipokuwa akitoa neno wakati akifungua kikao cha kupitia taarifa za Utekelezaji wa Mradi huo kilichohusisha timu ya wataalamu wa Utekelezaji wa Mradi, timu ya wataalamu kutoka Bank ya Dunia na Wajumbe wengine kutoka Taasisi mbalimbali na Wizara.

Dkt. Semesi amesema Mradi huo sio tu una manufaa katika kupunguza matumizi ya Zebaki lakini pia una faida nyingi zaidi.


"Matokeo tayari yanaonekana na yanasababisha mabadiliko katika sekta ya madini, ikiwa ni pamoja na matumizi ya teknolojia mbadala wa zebaki. EHPMP haihusu tu kupunguza matumizi ya zebaki; inahusu kubadilisha sekta ya uchimbaji mdogo wa dhahabu. Inalenga kulinda wachimbaji madini na familia zao, kukuza urasimishaji na utawala bora, kuimarisha utunzaji wa mazingira, na kuimarisha ustahimilivu wa kiuchumi. Hatimaye, inalenga kuhakikisha kwamba utajiri unaotokana na dhahabu ya Tanzania unaenda sambamba na matumizi salama ambayo yanalinda afya ya umma na mazingira." Amesema Dkt. Semesi.

Akizungumzia kuhusu Utekelezaji wa Mradi huo, Dkt. Semesi hakusita kusema kuhusu uratibu mzuri unaofanywa kwa kushirikiana baina ya NEMC na Benki ya Dunia hali iliyopelekea matokeo hayo chanya ya Utekelezaji wa Mradi huo.


"Kufikia leo, utekelezaji umefikia 84% ya vipengele vilivyopangwa, kuonyesha maendeleo makubwa kuelekea malengo ya mradi. Hii inajengwa juu ya msingi uliowekwa na Benki ya Dunia na NEMC kwa kuwa na usimamizi thabiti na kuhakikisha kwamba afua za mradi zinafikiwa kwa ufanisi zaidi." Ameongezea Dkt. Semesi.

Baraza la Taifa la Hifadhi na Usimamizi wa Mazingira (NEMC) limesimamia mradi huu wa miaka minne tangu Oktoba 2020 na umekuwa ukitekelezwa katika mikoa 7 ambayo ni Mwanza, Mara, Geita, Shinyanga, Singida, Mbeya na Songwe. Awali Mradi uliopangwa kufungwa Julai 2025, mradi umeongezwa hadi mwezi Machi, 2026 ili kuruhusu kukamilika kwa vipengele muhimu, ikiwa ni pamoja na ujenzi wa Kituo cha Uhamasishaji cha Zebaki na Kituo Mbadala cha Zebaki. Nyenzo hizi ni muhimu ili kuhakikisha kupitishwa kwa teknolojia salama, kukuza mbinu zisizo na zebaki, na kuanzishwa kwa Kituo cha Ubora.







NEMC NA TAASISI ZA KISERIKALI NA ZISIZO ZA KISERIKALI WAFANYA MAPITIO YA MPANGO KAZI WA BARAZA

Baraza la Taifa la Hifadhi na Usimamizi wa Mazingira (NEMC) kwa kushirikiana na wadau kutoka taasisi za kiserikali na zisizo za kiserikali wameshirikiana kutoa maoni kwenye Mpango mkakati mpya (Strategic Plan) wa Mwaka 2026/2027-2030/2031 ikiwa ni hatua mojawapo  ya kuhakikisha utendaji kazi wa Baraza wenye tija na manufaa kwa muktadha wa utunzaji wa Mazingira.

Akifungua Kikao hicho, Februari 3, 2026, Mkurugenzi wa Fedha na Utawala Bw. Dickson Mjinja kwa niaba ya Mkurugenzi Mkuu Dkt. Immaculate Sware Semesi aliwashukuru washiriki wote kwa kujitoa na kufika kwa wingi ili kufanikisha dhumuni la Kikao hicho muhimu chenye tija katika Utekelezaji wa majukumu ya Baraza.











NEMC YASHIRIKI KIKAMILIFU KONGAMANO LA ANWANI ZA MAKAZI NA MAONESHO YA TEKNOLOJIA ZA POSTA 2026

Baraza la Taifa la Hifadhi na Usimamizi wa Mazingira (NEMC) limeshiriki kikamilifu Kongamano la Mwaka la Anwani za Makazi na Maonesho ya Hud...