Nyumbani

MWENYEKITI WA BODI YA NEMC AZUNGUMZA NA WADAU WA MAZINGIRA, NEMC@40

Mwenyekiti wa Bodi ya NEMC, Mhandisi Mwanasha Tumbo akizungumza wakati wa Maadhimisho ya Miaka Arobaini (40) ya Baraza la Taifa la Hifadhi na Usimamizi wa Mazingira (NEMC) yaliyofanyika tarehe 29 Mei 2026 katika Ukumbi wa Mikutano wa Julius Nyerere (JNICC), Jijini Dar es Salaam.

Katika mazungumzo hayo, amesisitiza umuhimu wa ushirikiano wa wadau mbalimbali katika kulinda na kuhifadhi mazingira, akieleza kuwa mafanikio ya NEMC katika kipindi cha miaka 40 yamechangiwa kwa kiasi kikubwa na ushiriki wa serikali, sekta binafsi, taasisi na wananchi.

Aidha, ametoa wito wa kuendelea kuwekeza katika elimu ya mazingira, matumizi ya teknolojia na utekelezaji wa sheria ili kuhakikisha mazingira yanalindwa kwa manufaa ya kizazi cha sasa na vijavyo.









NEMC IMEADHIMISHA MIAKA 40 TANGU KUANZISHWA KWAKE MWAKA 1986

 Baraza la Taifa la Hifadhi na Usimamizi wa Mazingira (NEMC) Mei 29, 2026  limeadhimisha miaka arobaini (40) tangu kuanzishwa kwake mwaka 1986.

Maadhimisho hayo yamewakutanisha Viongozi mbalimbali wa ndani na nje ya Tanzania pamoja na wadau kutoka taasisi za umma na binafsi pamoja na mabalozi wa Mazingira ambayo yamekuwa jukwaa muhimu la kubadilishana uzoefu katika suala zima la Uhifadhi na Usimamizi wa Mazingira.

Akizungumza katika Maadhimisho hayo, Mkurugenzi Mkuu wa NEMC Dkt. Immaculate Sware Semesi alisema miaka arobaini (40) ya NEMC ni hatua mpya ya kutekeleza majukumu kwa nguvu mpya na ufanisi, amesema katika miaka yote hiyo Baraza limejufunza, limeimarika na lipo tayari kuendelea kulitumikia Taifa kwa weledi na uzalendo.






































NEMC YAMTUNUKU MHE. RAIS SAMIA TUZO YA MAZINGIRA

 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan ametunukiwa Tuzo maalum ya Mazingira kutokana na mchango wake mkubwa katika uhifadhi na usimamizi wa mazingira nchini.

Tuzo hiyo imekabidhiwa na Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar, Mhe. Hemed Suleiman Abdulla,  kwa niaba ya Rais Dkt. Samia katika kilele cha maadhimisho ya miaka 40 ya NEMC yaliyofanyika JNICC, jijini Dar es Salaam.

Aidha, tuzo hiyo imetolewa ikiwa ni kutambua juhudi za Dkt. Samia katika kuhamasisha matumizi ya nishati safi ya kupikia pamoja na kampeni za kupunguza uharibifu wa mazingira unaotokana na ukataji holela wa miti kwa ajili ya kuni na mkaa.

Kupitia juhudi hizo, Dkt. Samia ameendelea kuhimiza wananchi kutumia nishati safi ya kupikia ili kulinda mazingira, kupunguza ukataji holela wa miti na kukabiliana na mabadiliko ya tabianchi.

MAKAMU WA PILI WA RAIS WA ZANZIBAR NI MGENI RASMI KATIKA KILELE CHA MAADHIMISHO YA MIAKA 40 YA NEMC

Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar, Mhe. Hemed Suleiman Abdulla, mgeni rasmi Kilele cha Maadhimisho ya Miaka 40 ya Baraza la Taifa la Hifadhi na Usimamizi wa Mazingira (NEMC), yaliyofanyika Mei 29, 2026 katika Ukumbi wa Julius Nyerere International Convention Centre (JNICC), Jijini Dar es Salaam.

Akizungumza katika maadhimisho hayo, Mhe. Hemed ameipongeza NEMC kwa mchango wake mkubwa katika usimamizi na uhifadhi wa mazingira nchini kwa kipindi cha miaka 40 tangu kuanzishwa kwake. Amesema taasisi hiyo imeendelea kuwa chachu ya utoaji wa elimu ya mazingira, usimamizi wa sheria za mazingira pamoja na kuhamasisha jamii kushiriki katika shughuli za uhifadhi wa mazingira kwa maendeleo endelevu ya Taifa.

Aidha, amewataka Watanzania kuendelea kushiriki kikamilifu katika utunzaji wa mazingira kwa kuepuka vitendo vinavyosababisha uharibifu wa mazingira na uchafuzi wa mazingira. Amesisitiza kuwa ushirikiano kati ya Serikali, taasisi mbalimbali na wananchi ni muhimu katika kuhakikisha mazingira yanaendelea kulindwa kwa manufaa ya kizazi cha sasa na kijacho.













MAKAMU WA PILI WA RAIS WA ZANZIBAR AZINDUA KITABU CHA MIAKA 40 YA NEMC

 Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar, Mhe. Hemed Suleiman Abdulla amezindua Kitabu cha Miaka 40 cha Baraza la Taifa la Hifadhi na Usimamizi wa Mazingira (NEMC) katika Kilele cha Maadhimisho ya Miaka 40 ya Taasisi hiyo yaliyofanyika mei 29, 2026 katika Ukumbi wa Mikutano wa Julius Nyerere (JNICC), Jijini Dar es Salaam.

Akizungumza wakati wa hafla hiyo, Mhe, Hemed ameipongeza NEMC kwa mchango wake mkubwa katika uhifadhi na usimamizi wa Mazingira nchini kwa kipindi cha miaka 40. Aidha ameeleza kuwa, Taasisi hiyo imeendelea kuwa nguzo muhimu katika kuhamasisha matumizi endelevu ya rasilimali za mazingira na kukabiliana na changamoto za uchafuzi wa mazingira pamoja na mabadiliko ya tabianchi.

Katika hayo, amewataka Watanzania kuendelea kushiriki kikamilifu katika shughuli za utunzaji wa mazingira kwa manufaa ya kizazi cha sasa na kijacho, huku akisisitiza umuhimu wa ushirikiano kati ya Serikali, Taasisi binafsi na jamii katika kuhakikisha mazingira yanaendelea kuwa salama kwa maendeleo ya Taifa.






MWENYEKITI WA BODI YA NEMC AZUNGUMZA NA WADAU WA MAZINGIRA, NEMC@40

Mwenyekiti wa Bodi ya NEMC, Mhandisi Mwanasha Tumbo akizungumza wakati wa Maadhimisho ya Miaka Arobaini (40) ya Baraza la Taifa la Hifadhi n...