Nyumbani

BODI YA WAKURUGENZI NEMC YAFANYA MAPITIO YA MPANGO MKAKATI WA UTEKELEZAJI WA MIAKA MITANO

Bodi ya Wakurugenzi wa NEMC pamoja na Menejimenti wamefanya kikao katika Ukumbi wa Hoteli ya Adden Palace jijini Mwanza kufanya mapitio ya pamoja ya mpango mkakati wa utekelezaji wa Taasisi wa miaka mitano (NEMC Strategic Plan 2026-2030) kwa lengo la kutoa mwelekeo, vipaumbele na uhalisia wa utekelezaji wake katika kuleta matokeo chanya kwa Taifa. 

Kikao hicho kilichowakutanisha wataalamu kiliendeshwa na Mwenyekiti wa Bodi Mhandisi Mwanasha Tumbo, ambapo washiriki walipata fursa ya kujadili kwa kina vipaumbele vya kimkakati vinavyolenga kuimarisha Uhifadhi na Usimamizi endelevu wa mazingira, kuboresha mifumo ya kiutawala, kupongeza ufanisi wa matumizi ya rasilimali pamoja na kuimarisha utoaji wa huduma kwa wadau.

Aidha maono na dhamira ya Taasisi yaliendelea kusisitizwa kupitia mikakati inayochochea matumizi ya Sayansi, teknolojia na ushirikiano wa wadau wa maendeleo.

Kwa ujumla mapitio ya Mpango mkakati yamehakikisha kuwa mwelekeo wa Baraza unaendana kikamilifu na Dira ya Taifa ya Maendeleo 2050 pamoja na ilani ya Chama hususan katika kulinda mazingira kwa maendeleo endelevu, kukuza uchumi wa kijani na kuboresha ustawi wa jamii. 

Kupitia kikao hiki, Baraza limeonesha dhamira thabiti ya kuhakikisha Mpango mkakati unakuwa chombo hai cha kufanikisha malengo ya maendeleo ya Taifa kwa Sasa na vizazi vijavyo.







NEMC YAKIFUNGA KIWANDA CHA HOOTA KWA KUTOKUZINGATIA TARATIBU ZA KIMAZINGIRA

Baraza la Taifa la Hifadhi na Usimamizi wa Mazingira NEMC Leo Februari 9, 2026 limekifunga kiwanda cha urejelezaji wa taka za plastiki cha HOOTA kilichopo Kata ya Vikindu Mkoani Pwani kutokana na kutekeleza shughuli zake kinyume na taratibu za kimazingira.

Akizungumza mara baada ya timu ya wataalamu wa Mazingira kutoka NEMC kukagua kiwanda hicho,   Meneja Utekelezaji wa Sheria (NEMC) Mhandisi Luhuvilo  Mwamila ameeleza changamoto zilizobainika katika kiwanda hicho ikiwa ni Pamoja kuanzisha kiwanda bila kufanya Tathmini ya Athari kwa Mazingira (TAM) na kutokuwa na cheti cha Mazingira, kuanzisha kiwanda katikati ya makazi ya watu hivyo kuhatarisha usalama wa wakazi wa maeneo hayo, pia kukosa teknolojia madhubuti ya kudhibiti hewa ya kemikali inayosababishwa na uendeshaji wa kiwanda hicho, kukosekana kwa vifaa kinga kwa wafanyakazi na utiririshaji wa maji taka kwenye makazi ya watu bila kuyatibu.

Ameeleza kuwa, awali NEMC ilikagua kiwanda hicho na kutoa maelekezo ambayo kiwanda hicho kinatakiwa kuzingatia lakini hakikutekeleza maagizo hayo hivyo Baraza limechukua hatua ya kukifungia kiwanda hicho mpaka kitakapo tekeleza maelekezo yote yaliyotolewa na NEMC.


Ameongeza kuwa NEMC inaunga mkono uwekezaji nchini kwa kuwataka wawekezaji wote kufuata taratibu zote za Kimazingira zinazotolewa na NEMC zikiwemo kufanya Tathmini ya Athari kwa Mazingira na kupatiwa cheti Cha Mazingira.

Kwa upande wake, Kaimu Meneja wa Kanda ya Mashariki Kusini (NEMC) Bw. Noel Kikwale amezitaka Mamlaka zinazohisika na Mipango miji kutenga Maeneo maalumu ya viwanda na kuhakikisha wawekezaji wanafanya shughuli zao katika Maeneo hayo ili kuepuka changamoto za kimazingira na afya ya wananchi.


Ukaguzi huo ulihusisha wataalamu wa Mazingira kutoka NEMC wakiongozwa na Meneja wa Utekelezaji wa Sheria Mhandisi Bi. Luvilo Mwamila na Viongozi wa Kata ya Vikindu na wa Serikali za mitaa.









NEMC YASHIRIKI MAPOKEZI YA BALOZI LUVANDA OFISI YA MAKAMU WA RAIS – DAR ES SALAAM

Baraza la Taifa la Hifadhi na Usimamizi wa Mazingira (NEMC) limeshiriki katika hafla ya mapokezi ya Naibu Katibu Mkuu Ofisi ya Makamu wa Rais, (Mazingira), Mhe. Balozi Baraka Haran Luvanda, aliyepokelewa rasmi leo Februari 09, 2026 katika Ofisi za Makamu wa Rais baada ya kuapishwa Ikulu, jijini Dar es Salaam.

Naibu Katibu Mkuu Ofisi ya Makamu wa Rais, (Mazingira)Mhe. Balozi Baraka Haran Luvanda akipokea maua kutoka kwa Afisa Mazingira Mkuu Bi. Upendo Ntunguja wakati wa mapokezi katika Ofisi za Makamu wa Rais baada ya kuapishwa Ikulu, jijini Dar es Salaam.

Hafla hiyo ya mapokezi imeongozwa na Naibu Waziri Ofisi ya Makamu wa Rais (Muungano na Mazingira), Mhe. Dkt. Festo Dugange, pamoja na Viongozi na  Watendaji wa Taasisi zilizo chini ya Ofisi ya Makamu wa Rais.

Akizungumza wakati wa mapokezi hayo, Mhe. Dkt. Dugange alimkaribisha rasmi Balozi Luvanda huku akisisitiza umuhimu wa ushirikiano wa karibu kati ya Ofisi ya Makamu wa Rais na Taasisi zake katika kutekeleza agenda ya kitaifa ya Muungano na Uhifadhi wa Mazingira.

Kwa upande wake, Balozi Luvanda alishukuru kwa mapokezi mazuri aliyopatiwa na kuahidi kufanya kazi bega kwa bega na Taasisi zote zilizo chini ya Ofisi ya Makamu wa Rais, hususan katika kuimarisha Usimamizi na Uhifadhi wa mazingira nchini. 

Ameeleza kuwa, utekelezaji wa majukumu yake utaongozwa na maono ya Mheshimiwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, kwa kuzingatia Sera, Sheria na Mikakati ya Taifa inayolenga Maendeleo Endelevu.

Aidha, Balozi Luvanda ameeleza dhamira yake ya kutumia uzoefu alionao katika kuimarisha Usimamizi wa Muungano, kulinda na kuhifadhi mazingira, pamoja na kuhakikisha Dira ya Taifa ya Muungano na Mazingira inatekelezwa kwa manufaa ya kizazi cha sasa na kijacho.

Akizungumza kwa niaba ya Mkurugenzi Mkuu wa NEMC, Meneja wa Kanda ya Temeke, Bw. Abel Sembeka, alimpongeza Balozi Luvanda kwa kuteuliwa kwake na kumhakikishia ushirikiano wa karibu kutoka NEMC katika kutekeleza majukumu ya Usimamizi, Uhifadhi na ulinzi wa mazingira nchini.

Bw. Sembeka alieleza kuwa NEMC itaendelea kutoa ushauri wa kitaalamu, kusimamia utekelezaji wa Sheria za Mazingira, pamoja na kuimarisha elimu na uhamasishaji wa masuala ya mazingira kwa jamii na wadau mbalimbali, sambamba na mwelekeo na vipaumbele vya Dira ya Taifa ya 2050






NEMC YASHIRIKI KIKAMILIFU KONGAMANO LA ANWANI ZA MAKAZI NA MAONESHO YA TEKNOLOJIA ZA POSTA 2026

Baraza la Taifa la Hifadhi na Usimamizi wa Mazingira (NEMC) limeshiriki kikamilifu Kongamano la Mwaka la Anwani za Makazi na Maonesho ya Huduma za Posta kwa kutoa elimu ya Mazingira kwa wadau walioshiriki katika Kongamano hilo.

Kongamano hilo limehitishwa rasmi leo Februari 8, 2026 na Mgeni Rasmi Waziri wa Mawasiliano na Teknolojia ya Habari Mhe. Angellah Jasmine Mbelwa Kairuki (Mb) ambapo ameeleza umuhimu wa matumizi ya mfumo wa Anwani za Makazi (NAPA) na kusisitiza matumizi ya mfumo huo ili kuwezesha utambuzi wa makazi na Maeneo ambayo shughuli za kiuchumi zinazohitaji ufuatililiaji zinafanyika.

Kongamano hilo  lililobeba kauli mbiu isemayo "𝘼𝙣𝙬𝙖𝙣𝙞 𝙈𝙖𝙝𝙞𝙧𝙞 𝙣𝙖 𝙐𝙗𝙪𝙣𝙞𝙛𝙪 𝙬𝙖 𝙃𝙪𝙙𝙪𝙢𝙖 𝙯𝙖 𝙋𝙤𝙨𝙩𝙖 𝙠𝙬𝙖 𝙐𝙠𝙪𝙖𝙟𝙞 𝙅𝙪𝙢𝙪𝙞𝙨𝙝𝙞" lilianza Februari 5 na kuhitimishwa rasmi leo Februari 8, 2026 ambapo Kongamano hilo limefanyika kuanzia Februari katika Ukumbi wa  wa Kimataifa wa Julius Nyerere (JNICC) Jijini Dar es salaam.





𝗠𝗔𝗧𝗨𝗞𝗜𝗢 𝗞𝗔𝗧𝗜𝗞𝗔 𝗣𝗜𝗖𝗛𝗔-𝗞𝗢𝗡𝗚𝗔𝗠𝗔𝗡𝗢 𝗟𝗔 𝗠𝗪𝗔𝗞𝗔 𝗟𝗔 𝗔𝗡𝗪𝗔𝗡𝗜 𝗭𝗔 𝗠𝗔𝗞𝗔𝗭𝗜 𝗡𝗔 𝗠𝗔𝗢𝗡𝗘𝗦𝗛𝗢 𝗬𝗔 𝗧𝗘𝗞𝗡𝗢𝗟𝗢𝗝𝗜𝗔 𝗬𝗔 𝗛𝗨𝗗𝗨𝗠𝗔 𝗭𝗔 𝗣𝗢𝗦𝗧𝗔 𝟮𝟬𝟮𝟲

Elimu ya Mazingira ikiendelea kutolewa kwa wadau waliotembelea banda la NEMC katika Kongamano la Mwaka la Anwani za Makazi na Maonesho ya Teknolojia ya Huduma za Posta 2026 linalofanyika katika Ukumbi wa Mikutano wa Kimataifa wa Julius Nyerere (JNICC) Jijini Dar es salaam.

Maonesho hayo yenye kauli mbiu isemayo "𝘼𝙣𝙬𝙖𝙣𝙞 𝙈𝙖𝙝𝙞𝙧𝙞 𝙣𝙖 𝙐𝙗𝙪𝙣𝙞𝙛𝙪 𝙬𝙖 𝙃𝙪𝙙𝙪𝙢𝙖 𝙯𝙖 𝙋𝙤𝙨𝙩𝙖 𝙠𝙬𝙖 𝙐𝙠𝙪𝙖𝙟𝙞 𝙅𝙪𝙢𝙪𝙞𝙨𝙝𝙞" yanatarajiwa kuhitimishwa rasmi Februari 8, 2026.










NEMC YAUNGURUMA JNICC KONGAMANO LA ANWANI ZA MAKAZI

Yatoa Elimu ya Uhifadhi na Usimamizi wa Mazingira 

Baraza la Taifa la Hifadhi na Usimamizi wa Mazingira (NEMC) limetoa elimu ya mazingira kwenye Kongamano la Mwaka la Anwani za Makazi na Maonesho ya Teknolojia ya Huduma za Posta 2026 ihusuyo masuala mazima ya uhifadhi na usimamizi wa mazingira kwa mujibu wa Sheria ya Mazingira ya Mwaka 2004 na Kanuni zake katika  Kituo cha Kimataifa cha Mikutano cha Julius Nyerere (JNICC), jijini Dar es Salaam.

Akizungumza katika kongamano hilo linalotarajiwa kuhitimishwa Februari 08, 2026, Mhandisi Mkuu wa NEMC Bw. Jampyon Mbugi amesema kuwa matumizi sahihi ya anwani za makazi ni nyenzo muhimu katika kuimarisha usimamizi wa mazingira kupitia mfumo wa NAPA ambao utaiwezesha NEMC kupata taarifa muhimu za uhifadhi na usimamizi wa mazingira.

Ameongeza kuwa elimu hiyo inalenga kuwajengea wananchi uelewa wa majukumu yao ya kisheria na kijamii katika kulinda mazingira. Hata hivyo, anwani za makazi si utambulisho pekee wa maeneo bali ni chombo muhimu cha kupanga makazi na kusimamia mazingira kwa maendeleo yanayozingatia ustawi wa jamii na mazingira kwa ujumla. 

Naye Mhandisi Migodi NEMC, Bw. Hezron Mwashibanda ameeleza kuwa huduma zinazotolewa katika banda la NEMC ni pamoja na udhibiti wa kelele chafuzi, ufuatiliaji wa utekelezaji wa Tathmini ya Athari kwa Mazingira (TAM/EIA), pamoja na utekelezaji wa Sheria, ada za mazingira katika maeneo ya makazi na biashara.

NEMC inawakaribisha wananchi na wadau wote wa mazingira kupata elimu ya uhifadhi na usimamizi wa mazingira.



NEMC YASHIRIKI MAFUNZO YA REMOTE SENSING NA GIS

 Baraza la Taifa la Hifadhi na Usimamizi wa Mazingira (NEMC) limeshiriki katika mafunzo ya matumizi ya teknolojia ya Remote Sensing na Geographic Information Systems (GIS) yanayolenga kuimarisha uwezo wa taasisi za Serikali katika usimamizi, ufuatiliaji na uhifadhi wa rasilimali za bahari na uvuvi yanayofanyika kwa muda wa siku nne kuanzia Februari 3 hadi 6, 2026, jijini Dar es Salaam. 

Mafunzo hayo yameratibiwa na Korean Institute of Ocean Science and Technology (KIOST) kwa kushirikiana na Taasisi ya Utafiti wa Uvuvi Tanzania (TAFIRI) huku wadau zaidi ya 20 kutoka sekta ya Bahari na Uvuvi wanaotoka katika taasisi mbalimbali za Serikali zimeshiriki mafunzo hayo ikiwa ni pamoja na Baraza la Taifa la Hifadhi na Usimamizi wa Mazingira (NEMC), Taasisi ya Utafiti wa Uvuvi Tanzania (TAFIRI), Taasisi ya Utafiti wa Uvuvi Zanzibar (ZAFIRI), Dar es Salaam Maritime Institute (DMI), Chuo Kikuu cha Dar es Salaam (UDSM), Fisheries Education and Training Agency (FETA), Mamlaka ya Hali ya Hewa Tanzania (TMA), Deep Sea Fishing Authority (DSFA), pamoja na Wizara ya Mifugo na Uvuvi (MLF).

Aidha, Mafunzo haya ni sehemu ya jitihada za kuimarisha matumizi ya teknolojia ya satelaiti katika ukusanyaji na uchambuzi wa taarifa zitakazosaidia katika usimamizi endelevu wa rasilimali za bahari na uvuvi, pamoja na kukabiliana na athari za mabadiliko ya tabianchi.






BODI YA WAKURUGENZI NEMC YAFANYA MAPITIO YA MPANGO MKAKATI WA UTEKELEZAJI WA MIAKA MITANO

Bodi ya Wakurugenzi wa NEMC pamoja na Menejimenti wamefanya kikao katika Ukumbi wa Hoteli ya Adden Palace jijini Mwanza kufanya mapitio ya p...