Nyumbani

SIKU 100 ZA SAMIA NA MAZINGIRA: Mageuzi, Uwajibikaji na Mustakabali wa Kijani kwa Tanzania




MazingiraYetuUhaiWetu Tuyatunze, Yatutunze

Katika kipindi cha siku 100 tangu kuingia madarakani kwa Samia Suluhu Hassan, Tanzania imeshuhudia kasi mpya ya mageuzi katika sekta ya mazingira. Chini ya uongozi wake, dhamira ya kulinda rasilimali za asili imewekwa katika mstari wa mbele wa ajenda ya maendeleo ya Taifa.

Kupitia Baraza la Taifa la Hifadhi na Usimamizi wa Mazingira (NEMC), Serikali imeonesha kwa vitendo kuwa maendeleo ya kweli hayawezi kutenganishwa na uhifadhi wa mazingira. Kauli mbiu #MazingiraYetuUhaiWetu si maneno tu ni mwito wa kitaifa wa kuchukua hatua sasa kwa ajili ya kizazi cha leo na kesho.

NEMC: Safari ya Kuwa Mamlaka Kamili ya Mazingira kuelekea Dira ya 2050

Katika safari ya kufikia Dira ya Taifa ya Maendeleo ya 2050, NEMC inaendelea kuimarishwa ili kuwa mamlaka kamili ya usimamizi wa mazingira nchini. Hatua hii ni ya kimkakati ikiipa taasisi nguvu zaidi za kisheria, kiutendaji na kiusimamizi.

Kadri miradi ya kimkakati, viwanda, uchimbaji madini na ujenzi wa miundombinu inavyoongezeka, ndivyo changamoto za kimazingira zinavyoongezeka pia. Kuifanya NEMC kuwa mamlaka kamili kutarahisisha:

· Uamuzi wa haraka na sahihi

· Utekelezaji madhubuti wa Sheria ya Mazingira

· Ufuatiliaji na ukaguzi wa miradi kwa ufanisi

· Kupunguza mwingiliano wa majukumu kati ya taasisi

Hii ni hatua ya kuwekeza katika uchumi imara unaoheshimu rasilimali za asili.

Utekelezaji Imara wa Sheria ya Mazingira

Katika siku 100, NEMC imekagua jumla ya miradi 648 nchini kote. Lengo? Kuhakikisha kila mradi unatekelezwa kwa kuzingatia misingi ya uhifadhi wa mazingira na kulinda afya za wananchi.

Mafanikio yaliyopatikana ni pamoja na:

· Tani 3,775.61 za taka hatarishi kuteketezwa kwa usalama

· Tani 74.40 za taka kurejelezwa

· Lita 722,500 za mafuta machafu kuchakatwa upya

Hatua hizi zimeimarisha uwajibikaji wa wawekezaji na kuonesha kuwa ukuaji wa uchumi unaweza kwenda sambamba na utunzaji wa mazingira.

Maboresho ya Tathmini ya Athari kwa Mazingira (TAM)

Huduma za Tathmini ya Athari kwa Mazingira na Jamii (TAM/EIA) zimeboreshwa kwa kupunguza muda wa uchakataji wa maombi bila kupunguza viwango vya kitaaluma.

Katika kipindi hiki:

· Miradi 381 yenye thamani ya trilioni 1.83 ilisajiliwa

· Miradi 362 iliidhinishwa baada ya kukidhi matakwa ya kisheria

Kwa kushirikiana na Institute of Resource Assessment ya Chuo Kikuu cha Dar es Salaam, NEMC inaendelea kuboresha mifumo yake ili kuongeza uwazi, ufanisi na ubora wa huduma.

Ushirikiano wa Kitaifa na Kimataifa

Mageuzi haya yameenda sambamba na kuimarishwa kwa ushirikiano na taasisi mbalimbali, ikiwemo:

· WaterAid  Usimamizi wa miradi ya maji kwa kuzingatia mazingira

· UPS – Mfumo wa kidigitali wa ufuatiliaji wa uchafuzi

· Chuo Kikuu cha Mzumbe  Tafiti za mazingira

· Centre for Science and Environment (CSE)  Udhibiti wa taka mijini na Ziwa Victoria

· Mamlaka ya Hali ya Hewa Tanzania (TMA)   Tafiti za mabadiliko ya tabianchi

Ushirikiano huu unaimarisha uwezo wa kitaifa kwa kutumia teknolojia, tafiti na utaalamu wa hali ya juu.

Elimu na Uhamasishaji: Jamii Kwanza

Katika kukuza ushiriki wa wananchi, NEMC imeendesha kampeni kabambe za uhamasishaji:

· Infographics 105

· Machapisho 161 ya kidigitali

· Vipindi 14 vya redio

· Vipindi 6 vya televisheni

· Habari 88 magazetini

Kupitia mitandao ya kijamii na majukwaa ya kidigitali, maelfu ya Watanzania wamefikiwa na kuelimishwa kuhusu haki na wajibu wao katika kulinda mazingira.

Kukabiliana na Mabadiliko ya Tabianchi

Katika ajenda ya mabadiliko ya tabianchi, NEMC inatekeleza miradi katika maeneo mbalimbali ikiwemo Dodoma, Singida, Tabora, Mara na Zanzibar, kwa lengo la:

· Kuimarisha ustahimilivu wa jamii

· Kulinda mifumo ikolojia

· Kupunguza athari za kemikali hatarishi

Mradi wa kudhibiti matumizi ya zebaki kwa wachimbaji wadogo wa dhahabu katika mikoa saba ni mfano wa juhudi za kulinda afya za wananchi na mazingira.

Utawala Bora na Uwajibikaji

Kwa kuendana na maelekezo ya Rais kuhusu nidhamu na uwajibikaji, NEMC ime:

· Kuboresha mifumo ya ndani ya usimamizi

· Kuimarisha Kamati ya Maadili

· Kutoa mafunzo ya maadili kwa watumishi

Hatua hizi zimeongeza uwazi, ufanisi na kuimarisha imani ya wananchi kwa taasisi.

Mazingira ni Uhai, ni Uchumi, ni Mustakabali

Siku 100 za Rais Samia katika sekta ya mazingira zimeweka msingi imara wa mageuzi yanayolenga maendeleo endelevu. Kuimarishwa kwa NEMC, utekelezaji wa sheria, ushirikiano mpana na uhamasishaji wa umma ni dalili kuwa Tanzania inaelekea katika uchumi wa kijani na maendeleo jumuishi.

Ni wajibu wetu sote kutambua kuwa:

Mazingira si chaguo  ni msingi wa maisha yetu.

#MazingiraYetuUhaiWetu
Tuyatunze, Yatutunze.

 


 

BODI YA WAKURUGENZI NEMC YAFANYA MAPITIO YA MPANGO MKAKATI WA UTEKELEZAJI WA MIAKA MITANO

Bodi ya Wakurugenzi wa NEMC pamoja na Menejimenti wamefanya kikao katika Ukumbi wa Hoteli ya Adden Palace jijini Mwanza kufanya mapitio ya pamoja ya mpango mkakati wa utekelezaji wa Taasisi wa miaka mitano (NEMC Strategic Plan 2026-2030) kwa lengo la kutoa mwelekeo, vipaumbele na uhalisia wa utekelezaji wake katika kuleta matokeo chanya kwa Taifa. 

Kikao hicho kilichowakutanisha wataalamu kiliendeshwa na Mwenyekiti wa Bodi Mhandisi Mwanasha Tumbo, ambapo washiriki walipata fursa ya kujadili kwa kina vipaumbele vya kimkakati vinavyolenga kuimarisha Uhifadhi na Usimamizi endelevu wa mazingira, kuboresha mifumo ya kiutawala, kupongeza ufanisi wa matumizi ya rasilimali pamoja na kuimarisha utoaji wa huduma kwa wadau.

Aidha maono na dhamira ya Taasisi yaliendelea kusisitizwa kupitia mikakati inayochochea matumizi ya Sayansi, teknolojia na ushirikiano wa wadau wa maendeleo.

Kwa ujumla mapitio ya Mpango mkakati yamehakikisha kuwa mwelekeo wa Baraza unaendana kikamilifu na Dira ya Taifa ya Maendeleo 2050 pamoja na ilani ya Chama hususan katika kulinda mazingira kwa maendeleo endelevu, kukuza uchumi wa kijani na kuboresha ustawi wa jamii. 

Kupitia kikao hiki, Baraza limeonesha dhamira thabiti ya kuhakikisha Mpango mkakati unakuwa chombo hai cha kufanikisha malengo ya maendeleo ya Taifa kwa Sasa na vizazi vijavyo.







NEMC YAKIFUNGA KIWANDA CHA HOOTA KWA KUTOKUZINGATIA TARATIBU ZA KIMAZINGIRA

Baraza la Taifa la Hifadhi na Usimamizi wa Mazingira NEMC Leo Februari 9, 2026 limekifunga kiwanda cha urejelezaji wa taka za plastiki cha HOOTA kilichopo Kata ya Vikindu Mkoani Pwani kutokana na kutekeleza shughuli zake kinyume na taratibu za kimazingira.

Akizungumza mara baada ya timu ya wataalamu wa Mazingira kutoka NEMC kukagua kiwanda hicho,   Meneja Utekelezaji wa Sheria (NEMC) Mhandisi Luhuvilo  Mwamila ameeleza changamoto zilizobainika katika kiwanda hicho ikiwa ni Pamoja kuanzisha kiwanda bila kufanya Tathmini ya Athari kwa Mazingira (TAM) na kutokuwa na cheti cha Mazingira, kuanzisha kiwanda katikati ya makazi ya watu hivyo kuhatarisha usalama wa wakazi wa maeneo hayo, pia kukosa teknolojia madhubuti ya kudhibiti hewa ya kemikali inayosababishwa na uendeshaji wa kiwanda hicho, kukosekana kwa vifaa kinga kwa wafanyakazi na utiririshaji wa maji taka kwenye makazi ya watu bila kuyatibu.

Ameeleza kuwa, awali NEMC ilikagua kiwanda hicho na kutoa maelekezo ambayo kiwanda hicho kinatakiwa kuzingatia lakini hakikutekeleza maagizo hayo hivyo Baraza limechukua hatua ya kukifungia kiwanda hicho mpaka kitakapo tekeleza maelekezo yote yaliyotolewa na NEMC.


Ameongeza kuwa NEMC inaunga mkono uwekezaji nchini kwa kuwataka wawekezaji wote kufuata taratibu zote za Kimazingira zinazotolewa na NEMC zikiwemo kufanya Tathmini ya Athari kwa Mazingira na kupatiwa cheti Cha Mazingira.

Kwa upande wake, Kaimu Meneja wa Kanda ya Mashariki Kusini (NEMC) Bw. Noel Kikwale amezitaka Mamlaka zinazohisika na Mipango miji kutenga Maeneo maalumu ya viwanda na kuhakikisha wawekezaji wanafanya shughuli zao katika Maeneo hayo ili kuepuka changamoto za kimazingira na afya ya wananchi.


Ukaguzi huo ulihusisha wataalamu wa Mazingira kutoka NEMC wakiongozwa na Meneja wa Utekelezaji wa Sheria Mhandisi Bi. Luvilo Mwamila na Viongozi wa Kata ya Vikindu na wa Serikali za mitaa.









NEMC YASHIRIKI MAPOKEZI YA BALOZI LUVANDA OFISI YA MAKAMU WA RAIS – DAR ES SALAAM

Baraza la Taifa la Hifadhi na Usimamizi wa Mazingira (NEMC) limeshiriki katika hafla ya mapokezi ya Naibu Katibu Mkuu Ofisi ya Makamu wa Rais, (Mazingira), Mhe. Balozi Baraka Haran Luvanda, aliyepokelewa rasmi leo Februari 09, 2026 katika Ofisi za Makamu wa Rais baada ya kuapishwa Ikulu, jijini Dar es Salaam.

Naibu Katibu Mkuu Ofisi ya Makamu wa Rais, (Mazingira)Mhe. Balozi Baraka Haran Luvanda akipokea maua kutoka kwa Afisa Mazingira Mkuu Bi. Upendo Ntunguja wakati wa mapokezi katika Ofisi za Makamu wa Rais baada ya kuapishwa Ikulu, jijini Dar es Salaam.

Hafla hiyo ya mapokezi imeongozwa na Naibu Waziri Ofisi ya Makamu wa Rais (Muungano na Mazingira), Mhe. Dkt. Festo Dugange, pamoja na Viongozi na  Watendaji wa Taasisi zilizo chini ya Ofisi ya Makamu wa Rais.

Akizungumza wakati wa mapokezi hayo, Mhe. Dkt. Dugange alimkaribisha rasmi Balozi Luvanda huku akisisitiza umuhimu wa ushirikiano wa karibu kati ya Ofisi ya Makamu wa Rais na Taasisi zake katika kutekeleza agenda ya kitaifa ya Muungano na Uhifadhi wa Mazingira.

Kwa upande wake, Balozi Luvanda alishukuru kwa mapokezi mazuri aliyopatiwa na kuahidi kufanya kazi bega kwa bega na Taasisi zote zilizo chini ya Ofisi ya Makamu wa Rais, hususan katika kuimarisha Usimamizi na Uhifadhi wa mazingira nchini. 

Ameeleza kuwa, utekelezaji wa majukumu yake utaongozwa na maono ya Mheshimiwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, kwa kuzingatia Sera, Sheria na Mikakati ya Taifa inayolenga Maendeleo Endelevu.

Aidha, Balozi Luvanda ameeleza dhamira yake ya kutumia uzoefu alionao katika kuimarisha Usimamizi wa Muungano, kulinda na kuhifadhi mazingira, pamoja na kuhakikisha Dira ya Taifa ya Muungano na Mazingira inatekelezwa kwa manufaa ya kizazi cha sasa na kijacho.

Akizungumza kwa niaba ya Mkurugenzi Mkuu wa NEMC, Meneja wa Kanda ya Temeke, Bw. Abel Sembeka, alimpongeza Balozi Luvanda kwa kuteuliwa kwake na kumhakikishia ushirikiano wa karibu kutoka NEMC katika kutekeleza majukumu ya Usimamizi, Uhifadhi na ulinzi wa mazingira nchini.

Bw. Sembeka alieleza kuwa NEMC itaendelea kutoa ushauri wa kitaalamu, kusimamia utekelezaji wa Sheria za Mazingira, pamoja na kuimarisha elimu na uhamasishaji wa masuala ya mazingira kwa jamii na wadau mbalimbali, sambamba na mwelekeo na vipaumbele vya Dira ya Taifa ya 2050






NEMC YASHIRIKI KIKAMILIFU KONGAMANO LA ANWANI ZA MAKAZI NA MAONESHO YA TEKNOLOJIA ZA POSTA 2026

Baraza la Taifa la Hifadhi na Usimamizi wa Mazingira (NEMC) limeshiriki kikamilifu Kongamano la Mwaka la Anwani za Makazi na Maonesho ya Huduma za Posta kwa kutoa elimu ya Mazingira kwa wadau walioshiriki katika Kongamano hilo.

Kongamano hilo limehitishwa rasmi leo Februari 8, 2026 na Mgeni Rasmi Waziri wa Mawasiliano na Teknolojia ya Habari Mhe. Angellah Jasmine Mbelwa Kairuki (Mb) ambapo ameeleza umuhimu wa matumizi ya mfumo wa Anwani za Makazi (NAPA) na kusisitiza matumizi ya mfumo huo ili kuwezesha utambuzi wa makazi na Maeneo ambayo shughuli za kiuchumi zinazohitaji ufuatililiaji zinafanyika.

Kongamano hilo  lililobeba kauli mbiu isemayo "𝘼𝙣𝙬𝙖𝙣𝙞 𝙈𝙖𝙝𝙞𝙧𝙞 𝙣𝙖 𝙐𝙗𝙪𝙣𝙞𝙛𝙪 𝙬𝙖 𝙃𝙪𝙙𝙪𝙢𝙖 𝙯𝙖 𝙋𝙤𝙨𝙩𝙖 𝙠𝙬𝙖 𝙐𝙠𝙪𝙖𝙟𝙞 𝙅𝙪𝙢𝙪𝙞𝙨𝙝𝙞" lilianza Februari 5 na kuhitimishwa rasmi leo Februari 8, 2026 ambapo Kongamano hilo limefanyika kuanzia Februari katika Ukumbi wa  wa Kimataifa wa Julius Nyerere (JNICC) Jijini Dar es salaam.





𝗠𝗔𝗧𝗨𝗞𝗜𝗢 𝗞𝗔𝗧𝗜𝗞𝗔 𝗣𝗜𝗖𝗛𝗔-𝗞𝗢𝗡𝗚𝗔𝗠𝗔𝗡𝗢 𝗟𝗔 𝗠𝗪𝗔𝗞𝗔 𝗟𝗔 𝗔𝗡𝗪𝗔𝗡𝗜 𝗭𝗔 𝗠𝗔𝗞𝗔𝗭𝗜 𝗡𝗔 𝗠𝗔𝗢𝗡𝗘𝗦𝗛𝗢 𝗬𝗔 𝗧𝗘𝗞𝗡𝗢𝗟𝗢𝗝𝗜𝗔 𝗬𝗔 𝗛𝗨𝗗𝗨𝗠𝗔 𝗭𝗔 𝗣𝗢𝗦𝗧𝗔 𝟮𝟬𝟮𝟲

Elimu ya Mazingira ikiendelea kutolewa kwa wadau waliotembelea banda la NEMC katika Kongamano la Mwaka la Anwani za Makazi na Maonesho ya Teknolojia ya Huduma za Posta 2026 linalofanyika katika Ukumbi wa Mikutano wa Kimataifa wa Julius Nyerere (JNICC) Jijini Dar es salaam.

Maonesho hayo yenye kauli mbiu isemayo "𝘼𝙣𝙬𝙖𝙣𝙞 𝙈𝙖𝙝𝙞𝙧𝙞 𝙣𝙖 𝙐𝙗𝙪𝙣𝙞𝙛𝙪 𝙬𝙖 𝙃𝙪𝙙𝙪𝙢𝙖 𝙯𝙖 𝙋𝙤𝙨𝙩𝙖 𝙠𝙬𝙖 𝙐𝙠𝙪𝙖𝙟𝙞 𝙅𝙪𝙢𝙪𝙞𝙨𝙝𝙞" yanatarajiwa kuhitimishwa rasmi Februari 8, 2026.










NEMC YAUNGURUMA JNICC KONGAMANO LA ANWANI ZA MAKAZI

Yatoa Elimu ya Uhifadhi na Usimamizi wa Mazingira 

Baraza la Taifa la Hifadhi na Usimamizi wa Mazingira (NEMC) limetoa elimu ya mazingira kwenye Kongamano la Mwaka la Anwani za Makazi na Maonesho ya Teknolojia ya Huduma za Posta 2026 ihusuyo masuala mazima ya uhifadhi na usimamizi wa mazingira kwa mujibu wa Sheria ya Mazingira ya Mwaka 2004 na Kanuni zake katika  Kituo cha Kimataifa cha Mikutano cha Julius Nyerere (JNICC), jijini Dar es Salaam.

Akizungumza katika kongamano hilo linalotarajiwa kuhitimishwa Februari 08, 2026, Mhandisi Mkuu wa NEMC Bw. Jampyon Mbugi amesema kuwa matumizi sahihi ya anwani za makazi ni nyenzo muhimu katika kuimarisha usimamizi wa mazingira kupitia mfumo wa NAPA ambao utaiwezesha NEMC kupata taarifa muhimu za uhifadhi na usimamizi wa mazingira.

Ameongeza kuwa elimu hiyo inalenga kuwajengea wananchi uelewa wa majukumu yao ya kisheria na kijamii katika kulinda mazingira. Hata hivyo, anwani za makazi si utambulisho pekee wa maeneo bali ni chombo muhimu cha kupanga makazi na kusimamia mazingira kwa maendeleo yanayozingatia ustawi wa jamii na mazingira kwa ujumla. 

Naye Mhandisi Migodi NEMC, Bw. Hezron Mwashibanda ameeleza kuwa huduma zinazotolewa katika banda la NEMC ni pamoja na udhibiti wa kelele chafuzi, ufuatiliaji wa utekelezaji wa Tathmini ya Athari kwa Mazingira (TAM/EIA), pamoja na utekelezaji wa Sheria, ada za mazingira katika maeneo ya makazi na biashara.

NEMC inawakaribisha wananchi na wadau wote wa mazingira kupata elimu ya uhifadhi na usimamizi wa mazingira.



SIKU 100 ZA SAMIA NA MAZINGIRA: Mageuzi, Uwajibikaji na Mustakabali wa Kijani kwa Tanzania

MazingiraYetuUhaiWetu Tuyatunze, Yatutunze Katika kipindi cha siku 100 tangu kuingia madarakani kwa Samia Suluhu Hassan, Tanzania imeshuhudi...