Baraza la Taifa la Hifadhi na Usimamizi wa Mazingira (NEMC) limeshiriki kikamilifu kilele cha Maadhimisho ya Siku ya Mazingira Duniani yaliyofanyika tarehe 5 Juni 2026 katika Ukumbi wa Mikutano wa Jakaya Kikwete (JKCC) Jijini Dodoma.
Maadhimisho hayo, yanayofanyika kila mwaka tarehe 5 Juni, kwa mwaka huu yaliadhimishwa kitaifa kwa kauli mbiu isemayo “Dira 2050: Tuwajibike Kukijanisha Tanzania”.