Waziri wa Nchi, Ofisi ya Makamu wa Rais (Muungano na Mazingira), Mhe. Mhandisi Hamad Y. Masauni, ameipongeza NEMC kwa kushirikiana na wadau wa mazingira katika juhudi za kubadili mtazamo wa jamii kuhusu taka na kuzigeuza kuwa fursa yenye manufaa ya kiuchumi na kimazingira.
Akizungumza katika maadhimisho ya Siku ya Kimataifa ya Kuondoa Taka Duniani yaliyofanyika leo, Machi 30, 2026, katika viwanja vya Mnazi Mmoja, Mhe. Masauni amesisitiza umuhimu wa kuendeleza dhana ya kupunguza, kutumia tena na kurejeleza taka (Reduce, Reuse, Recycle), sambamba na kauli mbiu ya mwaka huu isemayo “kupunguza taka katika sekta ya chakula.”
"Taka siyo uchafu bali ni fursa; tukizisimamia vizuri tunaweza kuzigeuza kuwa rasilimali yenye thamani kwa maendeleo endelevu.” Amesema Waziri Masauni.
Naye Mkuu wa Wilaya ya Ilala, Mhe. Edward Mpogolo, akimwakilisha Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, amesisitiza kuendelea kwa utoaji wa elimu ya mazingira hususan shuleni kuanzia ngazi ya msingi, pamoja na kuimarisha mafunzo kwa makampuni ya ukusanyaji taka kwa kushirikiana na NEMC ili kuongeza ufanisi katika sekta hiyo.
Kwa upande wake, Mkurugenzi Mkuu wa NEMC, Dkt. Immaculate Sware Semesi, amesisitiza umuhimu wa kuendelea kutoa elimu ya mazingira kwa jamii ili kuongeza uelewa juu ya usimamizi bora wa taka na kuchochea ushiriki wa wananchi katika kulinda mazingira.
Maadhimisho hayo yamefanyika kwa lengo la kuhamasisha jamii kutambua thamani ya taka na kuzitumia kama rasilimali kwa maendeleo endelevu, huku yakiwakutanisha wadau mbalimbali wa mazingira.
.jpeg)



.jpeg)
.jpeg)
.jpeg)


.jpeg)

.jpeg)

.jpeg)
.jpeg)













.jpeg)


