Nyumbani

 Baraza la Taifa la Hifadhi na Usimamizi wa Mazingira (NEMC) leo tarehe 26, Septemba, 2025 limefanya Kikao na wadau kutoka Benki ya Dunia ili kujadili fursa za mazingira zinazoweza kuchangia katika uongezaji wa thamani kwenye shughuli za utafiti, uchimbaji na uchenjuaji wa madini.

Majadiliano hayo yaliyoongozwa na Meneja wa NEMC-Kanda ya Ziwa Magharibi Bw. Boniface Guni ambayo yalilenga kutambua kwa ujumla majukumu ya NEMC na vipaumbele vyake katika sekta ya Madini.

Meneja wa NEMC-Kanda ya Ziwa Magharibi Bw. Boniface Guni (kulia) akizungumza katika Kikao hicho

Wataalamu kutoka Benki ya Dunia wakiwa katika Kikao hicho kilichofanyika tarehe 26, Septemba, 2025 katika Ukumbi wa Mikutano wa NEMC Jijini Dar es Salaam

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni

TIMU YA UKAGUZI WA MAZINGIRA KUTOKA NEMC MAKAO MAKUU NA KANDA YA ZIWA VICTORIA MASHARIKI WAADHIMISHA MEIMOSI 2026 KWA KUPANDA MITI MAKUMBUSHO YA MWL. JULIUS K. NYERERE, BUTIAMA

Timu ya watumishi wa Baraza la Taifa la Hifadhi na Usimamizi wa Mazingira (NEMC) wanaofanya ukaguzi wa mazingira katika mikoa ya Kanda ya Zi...