Nyumbani

NEMC, OFISI YA MAKAMU WA RAIS, WIZARA YA NISHATI NA PURA WATEMBELEA MAMLAKA YA MAZINGIRA NCHINI NORWAY KUJADILI NISHATI KWA MAENDELEO ENDELEVU

Pichani ni ujumbe wa Tanzania ukiwajumuisha maafisa kutoka Ofisi ya Makamu wa Rais, Baraza la Taifa la Hifadhi na Usimamizi wa Mazingira (NEMC), Wizara ya Nishati na PURA uliotembelea ofisi za Mamlaka ya Mazingira ya Norway (Norwegian Environment Agency-NEA) kubadilishana uzoefu na kujadili fursa za ushirikiano chini ya mpango wa Nishati kwa Maendeleo (Energy for Development).

Ziara hii imelenga kuimarisha ushirikiano katika udhibiti wa uchafuzi, taarifa za mabadiliko ya tabianchi na maendeleo yenye uzalishaji mdogo wa hewa chafuzi.

Kupitia mpango wa Nishati kwa Maendeleo (Energy for Development - EfD), NEA inashirikiana na nchi za Afrika zikiwemo Tanzania, Nigeria, Msumbiji, Malawi, Uganda, Ghana na Afrika Kusini. Ushirikiano wa sasa kati ya Tanzania na Norway unalenga udhibiti wa uchafuzi wa mazingira na utoaji wa taarifa za hali ya hewa, lakini unaweza kuongezwa baada ya mwaka 2026 kujumuisha maeneo mapana zaidi kama mabadiliko ya tabianchi, bayoanuai na usimamizi wa uchafuzi

Mamlaka ya Mazingira ya Norway (Norwegian Environment Agency - NEA) ndiyo taasisi kuu inayotekeleza sera za mazingira za Norway chini ya Wizara ya Hali ya Hewa na Mazingira. Muundo wake wa uongozi ni rahisi, Serikali, Wizara, NEA, Magavana na Halmashauri za Manispaa na inatoa ushauri kuhusu mabadiliko ya tabianchi, bayoanuai, uchafuzi wa mazingira na matumizi ya ardhi. NEA pia huandaa Ripoti za Hali ya Mazingira, hutoa kanuni na vibali, na kushirikiana kitaifa na kimataifa.

Mfumo wa kisheria wa Norway wa udhibiti wa hewa chafu unajumuisha Sheria ya Udhibiti wa Uchafuzi (Pollution Control Act, 1993), Usalama na Mazingira (HSE) kwa shughuli za mafuta na gesi, Kanuni za Uchafuzi na Taka, Vibali vya Udhibiti wa Uchafuzi, Sheria ya Biashara ya Uzalishaji wa Gesi Joto (Greenhouse Gas Emissions Trading Act), na Sheria ya Ulinzi wa Uanuai (Nature Diversity Act). Sheria hizi huipa NEA mamlaka ya kudhibiti utoaji wa gesi chafuzi kama methane na kabonidaioksaidi (CO2) na kuhakikisha ufuatiliaji na utekelezaji wa masharti kwa sekta mbalimbali, zikiwemo mafuta na taka.

Kwa kadirio la uzalishaji wa methane kutoka dampo na maeneo ya utupaji taka, NEA hutumia mbinu za Shirika la Kiserika

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni

NEMC YASHIRIKI MKUTANO WA SABA WA UMOJA WA MATAIFA KUHUSU MAZINGIRA

Baraza la Taifa la Hifadhi na Usimamizi wa Mazingira (NEMC) linashiriki Mkutano wa Saba (07) wa Umoja wa Mataifa kuhusu Mazingira (07th Unit...