Nyumbani

NEMC YASHIRIKI MKUTANO WA SABA WA UMOJA WA MATAIFA KUHUSU MAZINGIRA

Baraza la Taifa la Hifadhi na Usimamizi wa Mazingira (NEMC) linashiriki Mkutano wa Saba (07) wa Umoja wa Mataifa kuhusu Mazingira (07th United Nations Environment Assembly – UNEA-7) unaofanyika jijini Nairobi, Kenya kuanzia 08 hadi 12 Disemba 2025 

Baadhi ya masuala yanayojadiliwa katika Mkutano huu ni pamoja na Mazingira Asilia na Mabadiliko ya Tabianchi; Uchumi Mzunguko, Chemikali, Taka na Uchafuzi wa Mazingira; Utawala na Sheria; na Bajeti.

Mkutano huu unaoongozwa na Ofisi ya Makamu wa Rais – Idara ya Mazingira, awali ulitanguliwa na mkutano wa maandalizi wa Kamati ya wawakilishi uliofanyika jijini hapo tarehe 01 hadi 05 Disemba 2025 ambapo wakuu wa nchi wanachama watatoa hotuba katika mkutano huo.

Zaidi ya NEMC, washiriki wengine ni Pamoja na Mamlaka ya Maabara ya Mkemia Mkuu wa Serikali (GCLA) na Wakala wa Misitu (TFS) ambapo Kilele cha mkutano huu ni tarehe 11 na 12 Disemba 2025.

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni

NEMC YASHIRIKI MKUTANO WA SABA WA UMOJA WA MATAIFA KUHUSU MAZINGIRA

Baraza la Taifa la Hifadhi na Usimamizi wa Mazingira (NEMC) linashiriki Mkutano wa Saba (07) wa Umoja wa Mataifa kuhusu Mazingira (07th Unit...