Nyumbani

PICHA ZA MATUKIO KATIKA KONGAMANO LA UNESCO LA PROGRAMU YA BINADAMU NA HIFADHI HAI CHINA


NEMC na TANAPA katika Kikao cha Kimataifa cha Kamati ya Programu ya UNESCO ya Binadamu na Hifadhi Hai kinachofanyika jijini Hangzhou nchini China kuanzia tarehe 26-28 Septemba 2025. Pichani ni Mkurugenzi Mkuu wa Baraza la Taifa la Hifadhi na Usimamizi wa Mazingira, Dkt. Immaculate Sware Semesi (Kulia) na Meneja wa Tafiti za Mazingira, Dkt. Rose Sallema na Mr. Albert Mziray Kamishna Msaidizi wa Uhifadhi kutoka TANAPA
Mkurugenzi Mkuu wa NEMC Dkt. Immaculate Sware Semesi (wa pili kushoto) katika Ukumbi wa Kongamano hilo, kushoto kwake ni Meneja wa Tafiti za Mazingira (NEMC) Dkt. Rose Sallema pamoja na washiriki wengine wa Kongamano hilo lililofanyika Nchini China
Mkurugenzi Mkuu wa NEMC Dkt. Immaculate Sware Semesi (wa pili kulia) akiwa katika picha ya pamoja na baadhi ya wadau wa maendeleo mara baada ya majadiliano kuhusu uwezekano wa kupata Fursa za Miradi kwenye Hifadhi Hai katika Kongamano la Dunia la Programu ya UNESCO ya Binadamu na Hifadhi Hai lililofanyika jijini Hangzhou nchini China. Kulia kwake ni Meneja wa Tafiti za Mazingira (NEMC) Dkt. Rose Sallema

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni

NEMC YASHIRIKI MKUTANO WA SABA WA UMOJA WA MATAIFA KUHUSU MAZINGIRA

Baraza la Taifa la Hifadhi na Usimamizi wa Mazingira (NEMC) linashiriki Mkutano wa Saba (07) wa Umoja wa Mataifa kuhusu Mazingira (07th Unit...