Baraza la Taifa la Hifadhi na Usimamizi wa Mazingira (NEMC) limeshiriki Warsha ya Kikanda Jijini Kampala (EAC) inayohusu masuala ya upangaji wa maeneo ya ufugaji samaki katika ziwa Victoria.
Akiripoti kutokea Kampala Meneja kutoka NEMC Bw.Jarome Kayombo amesema warsa hiyo imelenga kuainisha vigezo vitalavyotumika kwa nchi zote tatu katika kupanga maeneo ya ufugaji, kutenga maeneo, kusimamia mazingira na usalama w Samaki.
Wajumbe walioshiriki kutoka Tanzania ni pamoja na Wizara ya Mifugo, NEMC, Bonde ziwa Victoria, Jumuia ya wafugaji Samaki, Umoja wa wavuvi, Vyuo vikuu pamoja na Tafiri.
Ujumbe ulioambatana na timu hiyo katika warsha umehusisha Uganda, Kenya, Tanzania, Burundi na Rwanda.
Meneja kutoka NEMC Bw. Jarome Kayombo (wa pili kulia) akiwa katika picha ya pamoja na washiriki wa Warsha ya Kikanda Jijini Kampala (EAC) inayohusu masuala ya upangaji wa maeneo ya ufugaji samaki katika ziwa Victoria.
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni