Kamishna wa Tume ya Utumishi wa Umma, Dkt. Laurean Ndumbaro (aliyesimama) akizungumza wakati wa kikao na watumishi wa NEMC alipozuru Ofisi za Baraza 23 Oktoba, 2025 ikiwa ni ziara yake ya kikazi
Akizungumza leo 23 Oktoba, 2025 jijini Dar es Salaam katika ziara yake ya kikazi ofisi za Baraza Dkt. Laurean Ndumbaro amesema uadilifu uliooneshwa na Baraza hilo ni mfano wa kuigwa na Taasisi nyingine za Umma katika kuhakikisha huduma kwa wananchi zinatolewa kwa ufanisi na kwa kuzingatia maadili ya kazi.
Mkurugenzi Mkuu wa NEMC Dkt. Immaculate Sware Semesi akizungumza wakati wa kikao hicho kilichokuwatanisha watumishi wa Baraza na Ugeni kutoka Tume ya Utumishi wa Umma ukiongozwa na Kamishna Dkt. Laurean Ndumbaro.
Amesisitiza kuwa uadilifu ndio nguzo kuu ya utumishi wa umma na ndio msingi wa kuaminika kwa Serikali mbele ya wananchi.
Ameongeza kuwa mafanikio ya NEMC katika utekelezaji wa miradi ya kimazingira pamoja na usimamizi wa Sheria na Kanuni za Mazingira ni ushahidi kwamba viongozi na watumishi wake wameweka maslahi ya Taifa mbele kuliko maslahi binafsi.
Mkurugenzi wa Miongozo, Uwezeshaji na Utafiti kutoka Tume ya Utumishi wa Umma Ndugu Peleleja Masesa akizungumza wakati wa kikao hicho.
Kwa upande wake Mkurugenzi Mkuu wa NEMC, Dkt. Immaculate Sware Semesi amemshukuru Kamishna kwa Tathmini hiyo na kuahidi kuendelea kufanya kazi kwa weledi, uadilifu na ubunifu zaidi kwani pongezi hizo ni chachu ya kuongeza ari ya watumishi kulinda rasilimali za Taifa na kuhakikisha maendeleo endelevu kwa vizazi vya sasa na vijavyo.
Katika ziara yake Kamishna Dkt. Ndumbaro ameambatana na wataalamu wengine akiwemo Mkurugenzi wa Miongozo, Uwezeshaji na Utafiti kutoka Tume ya Utumishi wa Umma Ndugu Peleleja Masesa.
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni