Katika kuadhimisha Wiki ya Huduma kwa Wateja, Baraza la Taifa la Hifadhi na Usimamizi wa Mazingira (NEMC) kupitia Ofisi ya Kanda ya Kati, leo tarehe 10 Oktoba, 2025, limetoa mafunzo kwa wakandarasi wa ujenzi waliosajiliwa na Bodi ya Usajili wa Makandarasi (CRB).
Mafunzo hayo yaliyofanyika katika Ofisi za Makao Makuu ya CRB, jengo la Mkandarasi House jijini Dodoma, yalilenga kuwaongezea wakandarasi uelewa kuhusu taratibu za Usimamizi wa Mazingira na umuhimu wa kutumia mifumo endelevu katika miradi ya ujenzi, ikiwemo udhibiti wa taka ngumu, taka maji na taka hatarishi.
Akizungumza wakati wa mafunzo hayo, Kaimu Meneja wa NEMC Kanda ya Kati, Bw. Novatus Mushi, alisisitiza umuhimu wa wakandarasi kuzingatia Tathmini ya Athari kwa Mazingira (TAM) na kufuata viwango vya ujenzi vinavyokidhi changamoto za kimazingira, hususan mabadiliko ya tabianchi yanayoweza kuathiri miundombinu.
Kaimu Meneja wa Kanda ya Kati (NEMC) Bw. Novatus Mushi akitoa elimu kwa Wakandarasi wa ujenzi katika mafunzo hayo
Baadhi ya wakandarasi wakifuatilia mafunzo hayo
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni