Nyumbani

NEMC NA WIOMSA WAENDESHA KONGAMANO LA WADAU WA BAHARI NCHINI KENYA

Timu ya wataalam wa Sayansi ya bahari kutoka Tanzania ikiongozwa na  Mkurugenzi Mkuu wa Baraza la Taifa la Hifadhi na Usimamizi wa Mazingira (NEMC) ambaye ni mratibu wa WIOMSA wameshiriki kongamano la wadau wa masuala ya bahari lililohusisha Watunga sera, wanasayansi ya bahari, wanasheria, wahandisi wa Mazingira, wanauchumi, wafanyabiashara, watafiti, wanavyuo na wazawa wanajamii ya pwani ambao ni wanachama wa Jumuiya ya Wanasayansi ya bahari magharibi mwa Bahari ya Hindi kwa lengo la kubadilishana uzoefu katika masuala ya Uhifadhi wa bahari ya Hindi.

Kongamano hilo la kumi na tatu (13 WIOMSA scientific symposium) limefanyika kuanzia tarehe 27 Septemba mpaka 3 Oktoba 2025 Mombasa nchini Kenya.

Timu ya NEMC ikiongozwa na Mkurugenzi Mkuu wa NEMC Dkt. Immaculate Sware Semesi na timu ya WIOMSA wakiwa katika picha ya pamoja mara baada ya awamu ya kwanza ya Kongamano hilo

Ushiriki wa Baraza kwenye kongamano hilo kumesaidia kuongeza  uelewa au kukuza taaluma ya Sayansi ya Bahari kwa wataalam wa bahari katika nyanja za Uhifadhi wa Mazingira, kupata fursa  za kukutana na wadau wanaotoa fedha za kusaidia miradi au tafiti za Mazingira ya Bahari na Bioanuai zake pamoja na kupata taasisi na mashirika mbalimbali ya kushirikiana katika tafiti na miradi ya Uhifadhi wa Mazingira ya Bahari.

Mkurugenzi Mkuu wa NEMC Dkt. Immaculate Sware Semesi akiwasilisha mada katika Kongamano hilo

Aidha ushiriki huo pia utasaidia kuanzisha na kuimarisha mashirikiano kati ya Maafisa/Wanasayansi ya Bahari katika nchi za ukanda wa Magharibi ya Bahari ya Hindi, kutambua fursa za uwekezaji katika tafiti, teknolojia, biashara na uwekezaji katika sekta ya Uchumi wa Buluu pamoja na  kuimarisha mahusiano ya kidiplomasia kati ya nchi wanachama wa WIOMSA.

Mkurugenzi Mkuu wa NEMC, Dkt. Immaculate Sware Semesi (wa pili kulia) akiwa na Mkurugenzi Mkuu wa WIOMSA Dkt.Arthur Tude na baadhi ya washiriki wa Kongamano hilo

Mawasilisho na majadiliano ya mada katika Kongamano hilo
Meneja wa Kanda ya Mashariki Kaskazini (NEMC) Bi. Glory Kombe akichangia mada wakati wa Kongamano hilo


Picha mbalimbali za washiriki wa Kongamano hilo zikijumuisha watumishi wa NEMC na wa WIOMSA 

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni

NEMC YASHIRIKI MKUTANO WA SABA WA UMOJA WA MATAIFA KUHUSU MAZINGIRA

Baraza la Taifa la Hifadhi na Usimamizi wa Mazingira (NEMC) linashiriki Mkutano wa Saba (07) wa Umoja wa Mataifa kuhusu Mazingira (07th Unit...