Nyumbani

NEMC YAADHIMISHA WIKI YA HUDUMA KWA MTEJA KWA VITENDO

Baraza la Taifa la Hifadhi na Usimamizi wa Mazingira (NEMC) katika kuadhimisha wiki ya huduma kwa mteja yenye kaulimbiu " Mission Possible" limeweka banda maalum katika ofisi zake ili kurahisisha  huduma kwa wateja wake moja kwa moja. 

Banda hilo limelenga kuboresha mawasiliano na kujenga mahusiano bora yenye kutoa fursa kwa wadau  kutoa maoni, changamoto, pamoja na kupatiwa majibu ya papo kwa papo kuhusu huduma za mazingira.

Mkurugenzi Mkuu wa NEMC, Dkt. Immaculate Sware Semesi akiwa katika banda maalum la kuhudumia wateja lililopo Ofisi za NEMC katika msimu wa Wiki ya Huduma kwa Mteja inayoadhimishwa kuanzia tarehe 6 hadi 10 Oktoba, 2025  

Wateja waliofika Ofisi za NEMC wakipatiwa huduma katika Wiki ya Huduma kwa Mteja 
Mkurugenzi wa Utawala na Fedha (NEMC) Bw. Dickson Mjinja akifuatilia utoaji wa huduma kwa wateja waliofika katika banda maalum la NEMC katika Maadhimisho ya Wiki ya huduma kwa Mteja 

Katika hatua nyingine Baraza Kupitia Kanda zake 13  limeendelea kutoa elimu ya Uhifadhi na Usimamizi wa Mazingira kwa wanachi

Ikiwa ni pamoja na kufanya ziara za ukaguzi (site visits) kwa wadau wake kujiridhisha na utekelezaji wa Kanuni za mazingira na kushughulikia changamoto zinazoibuliwa na wananchi


Hakuna maoni:

Chapisha Maoni

TIMU YA UKAGUZI WA MAZINGIRA KUTOKA NEMC MAKAO MAKUU NA KANDA YA ZIWA VICTORIA MASHARIKI WAADHIMISHA MEIMOSI 2026 KWA KUPANDA MITI MAKUMBUSHO YA MWL. JULIUS K. NYERERE, BUTIAMA

Timu ya watumishi wa Baraza la Taifa la Hifadhi na Usimamizi wa Mazingira (NEMC) wanaofanya ukaguzi wa mazingira katika mikoa ya Kanda ya Zi...