Baraza la Taifa la Hifadhi na Usimamizi wa Mazingira (NEMC) kupitia kurugenzi ya Tathmini ya Athari kwa Mazingira na Jamii imetoa mafunzo ya Tathmini ya Athari kwa Mazingira kwa wataalamu elekezi wa mazingira na watumishi wa Baraza waliopo Kanda ya Magharibi inayohusisha mikoa mitatu (Kigoma, Katavi na Tabora) kuanzia tarehe 1-3 Oktoba, 2025.
Mafunzo haya ni endelevu na lengo kuu ni kuboresha ufanyaji wa Tathmini ya Athari kwa Mazingira na Jamii (TAM) na upitiaji wa taarifa za TAM zinazowasilishwa Baraza.
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni