Baraza la Taifa la Hifadhi na usimamizi wa Mazingira (NEMC) kupitia Kurugenzi ya Utekelezajia na Uzingatiaji wa Sheria limeshiriki Mkutano wa tano wa Kimataifa unaohusu masuala ya taka za kielektroniki uliofanyika kuanzia tarehe 16 na 17 Oktoba, 2025 Mombasa, nchini Kenya.
Mkutano huo umewaleta pamoja wadau kutoka Serikalini, wadau wa Maendeleo, wataalamu, Sekta binafsi pamoja na asasi za kiraia ili kujadili kwa pamoja masuala yanahusu taka za kielektroniki.
Katika mkutano huo NEMC ilishiriki katika kutoa neno la ukaribisho pamoja na kusisitiza wadau kutumia jukwaa hilo la majadiliano vizuri ili kutatua changamoto na kuibua fursa ambazo zitaleta tija katika kuhifadhi mazingira, kuongeza ajira na kukuza uchumi rejeshi.
Meneja Utekelezaji wa Sheria (NEMC) Bi. Amina Kibola akiwasilisha mada katika Mkutano huo
"Lengo mahususi la mkutano huo ni kuoanisha Sera, Sheria, na mifumo ya Usimamizi wa taka hizo. Kujadili ukuaji wa teknolojia unaoenda sambamba na ongezeko kubwa la uzalishaji wa taka za kielektroniki.
Aidha, Uwekezaji, fursa na mbinu mbalimbali za uchakataji wa taka hizo pia ni eneo lililojadili na wadau.
Meneja Utekelezaji wa Sheria (NEMC) Bi. Amina Kibola akifuatilia uwasilishaji mada katika Mkutano huo, kulia kwake ni Mhandisi Bi. Beatitude Sizya
Timu ya NEMC iliyoshiriki Mkutano huo ikiwa katika picha ya pamoja na baadhi ya washiriki wa Mkutano huo
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni