Nyumbani

NEMC YASHIRIKI KIKAO CHA TEKNOLOJIA ZA UREJESHAJI MAZINGIRA NCHINI AUSTRIA

Baraza la Taifa la Hifadhi na Usimamizi wa Mazingira (NEMC) limeshiriki kikao cha kutathmini mapungufu na changamoto za teknolojia za kimazingira zinazotumika kwenye kurejesha mazingira yaliyoharibiwa au kuchafuliwa (remediation technologies).

Afisa Mazingira Mwandamizi Bi. Kuruthumu Shushu (wa pili kushoto) akiwa katika picha ya pamoja na baadhi ya washiriki wa kikao hicho
Kikao hicho kilifanyika katika makao makuu ya Shirika la Umoja wa Mataifa la Nishati ya Nyuklia (IAEA) yaliyopo jijini Vienna, Austria kuanzia tarehe 13-17 Oktoba, 2025.

Lengo la kikao ni kukutanisha wawakilishi kutoka nchi mbalimbali wanaohusika na Udhibiti na Tafiti katika Sekta ya Nishati ya nyuklia ili kujadili njia bora za urejeshaji wa mazingira yaliyoharibiwa au kuchafuliwa.

Njia mbalimbali za urejeshaji wa mazingira zilijadiliwa na nchi wanachama pamoja na mapungufu na changamoto zake na kujifunza njia bora inayoweza kutekelezwa na nchi husika.

Uwasilishaji wa mada ukifanyika katika kikao cha kutathmini mapungufu na changamoto za teknolojia za kimazingira zinazotumika kwenye kurejesha mazingira yaliyoharibiwa au kuchafuliwa (remediation technologies) kilichofanyika nchini Austria 

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni

NEMC YASHIRIKI MKUTANO WA SABA WA UMOJA WA MATAIFA KUHUSU MAZINGIRA

Baraza la Taifa la Hifadhi na Usimamizi wa Mazingira (NEMC) linashiriki Mkutano wa Saba (07) wa Umoja wa Mataifa kuhusu Mazingira (07th Unit...