Nyumbani

NEMC YATOA MAFUNZO YA TATHMINI YA ATHARI KWA MAZINGIRA KWA WANAFUNZI WA DARTU


Baraza la Taifa la Hifadhi na Usimamizi wa Mazingira (NEMC) limeendesha mafunzo maalum ya kuwajengea uelewa kuhusu Tathmini ya Athari kwa Mazingira (TAM) wanafunzi wa mwaka wa tatu wa kada ya ualimu kutoka Chuo Kikuu cha Tumaini Dar es Salaam (DARTU).

Mafunzo hayo yamefanyika leo, Julai 3, 2025, katika Ukumbi wa NEMC uliopo jijini Dar es Salaam, na yaliongozwa na Afisa Mazingira Mwandamizi, Bw. Emmanuel Salyeem.

Katika mafunzo hayo, Bw. Salyeem alitoa wasilisho lililojikita katika kuelezea mchakato mzima wa Tathmini ya Athari kwa Mazingira, akitoa mifano hai ya namna Baraza linaendesha tathmini hiyo kwenye miradi mikubwa, ya kati na midogo. Alisisitiza umuhimu wa TAM katika kulinda afya ya viumbe hai wote pamoja na mazingira kwa ujumla.

Kupitia mafunzo haya, wanafunzi walipata nafasi ya kuelewa kwa kina majukumu ya NEMC na mchango wa tathmini ya kimazingira katika maendeleo endelevu ya taifa.

NEMC inaendelea kutoa wito kwa taasisi za elimu, vikundi vya kijamii na wadau mbalimbali kufika katika ofisi za Baraza kwa ajili ya kupata elimu ya uhifadhi wa mazingira na kujifunza namna bora ya kushiriki katika kulinda mazingira yetu. 







 

Maoni 3 :

  1. Well done,your mostly welcome at water Institute . NEMC, we need education concerning environment.
    πŸ™πŸΏπŸ™πŸΏπŸ™πŸΏ

    JibuFuta

Sethi Ura Company Limited Yasimamia Mapinduzi ya Usafi: Ushirikiano wa Jamii Katika Kuweka Mazingira Safi Hospitali ya Wilaya ya Hai

Vijana wa kujitolea wakipanga majukumu kabla ya kuanza kazi ya usafi katika eneo la hospitali. Katika kuendeleza dhana ya afya bora inayoteg...