Nyumbani

NEMC YAWALETA PAMOJA WATUMISHI WAKE KUJIPANGA KWA MWAKA 2026

 Ni katika kufanya tathmini na kuimarisha umoja. 

Watumishi wa Baraza la Taifa la Hifadhi na Usimamizi wa Mazingira (NEMC) Makao Makuu na kutoka kanda zote 13 nchini, wamekutana katika eneo la Ndotopolepole, Wilaya ya Bagamoyo, katika hafla maalum iliyolenga kuimarisha mshikamano, kujengeana uelewa, kufanya tathmini fupi ya utendaji kazi na kufurahi pamoja, ikiwa pia ni sehemu ya kufunga mwaka 2025.

Akizungumza katika hafla hiyo, Mkurugenzi Mkuu wa NEMC, Dkt. Immaculate Sware Semesi, amewataka watumishi wa Baraza kudumisha umoja na mshikamano katika utendaji kazi (team building), kufanya kazi kwa bidii na kuongeza nidhamu pamoja na unadhifu wa kazi, kama nguzo muhimu za kufanikisha maono na dira ya Taasisi katika mwaka 2026.

Dkt. Semesi ameongeza kuwa katika kuboresha mazingira ya utendaji kazi, NEMC imejipanga kuimarisha matumizi ya mifumo ya kidigitali, ambapo tayari baadhi ya mifumo ya ufuatiliaji wa mazingira imeanza kutumika, hatua inayolenga kuongeza ufanisi na uwajibikaji katika kazi.

Hafla hiyo pia imehusisha utoaji wa zawadi kwa watumishi walioonesha utendaji kazi mzuri na bidii, ikiwa ni sehemu ya kuhamasisha ari, nidhamu na ushindani chanya mahali pa kazi.

Akitoa pongezi kwa wafanyakazi waliofanya vizuri, Dkt. Semesi aliipongeza menejimenti na watumishi wote wa NEMC kwa ujumla, na kuwasihi kuongeza bidii, ubunifu na ari mpya katika kutekeleza majukumu yao kwa mwaka 2026.

Aidha, hafla hiyo ilipambwa na michezo mbalimbali ya kujenga ushirikiano, mshikamano na moyo wa kutokata tamaa katika kazi, ambapo washindi walitunukiwa zawadi kama motisha.





















Hakuna maoni:

Chapisha Maoni

NEMC YAWALETA PAMOJA WATUMISHI WAKE KUJIPANGA KWA MWAKA 2026

  Ni katika kufanya tathmini na kuimarisha umoja.  Watumishi wa Baraza la Taifa la Hifadhi na Usimamizi wa Mazingira (NEMC) Makao Makuu na k...