Nyumbani

NEMC YATAMBUA USHIRIKIANO KATI YAKE NA JESHI LA POLISI

Yashiriki mahafali ya kumi ya programu za vyuo vya polisi

Baraza la Taifa la Hifadhi na Usimamizi wa Mazingira (NEMC) limetambua mchango wa jeshi la polisi ulionao katika Utekelezaji wa Sheria ya Mazingira hasa suala la ulinzi na usalama kwa maafisa wakati wa ukaguzi, kudhibiti ukaidi na kuhakikisha hatua za kisheria zinachukuliwa katika masuala ya Mazingira nchini.

Hayo yamedhihirika wakati wa mahafali ya kumi ya programu za vyuo vya polisi yaliyofanyika Januari 29, 2026 katika viwanja vya chuo cha taaluma ya polisi Jijini Dar es Salaam ambapo Mkurugenzi Mkuu wa NEMC Dkt.Immaculate Sware Semesi ameshiriki.

Ushiriki wake ni muhimu katika kutambua mchango ilionao wa kuimarisha utekelezaji wa Sheria za Mazingira nchini kwani uhalifu wa kimazingira kama kelele chafuzi, uharibifu wa mazingira na biashara haramu ya taka hudhibitiwa kwa ufanisi zaidi hali inayoongeza utii wa Sheria, kurahisisha uchunguzi na uwasilishaji wa kesi mahakamani.

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni

NEMC YATAMBUA USHIRIKIANO KATI YAKE NA JESHI LA POLISI

Yashiriki mahafali ya kumi ya programu za vyuo vya polisi Baraza la Taifa la Hifadhi na Usimamizi wa Mazingira (NEMC) limetambua mchango wa ...