Nyumbani

NEMC YAFANIKISHA MAFUNZO YA KUJENGEA UWEZO KITAIFA WIZARA, TAASISI NA MAMLAKA ZA SERIKALI ZA MITAA JUU YA NYENZO ZA USIMAMIZI WA MAZINGIRA

Baraza za la Taifa la Hifadhi na Usimamizi wa Mazingira NEMC limefanikisha mafunzo ya kujenga uwezo wa kitaifa juu ya nyenzo za Usimamizi wa Mazingira nchini kwa Wizara, Taasisi na Mamlaka za Serikali za mitaa.

Mafunzo hayo ya siku mbili   yalianza jana 20 Agosti, hadi leo 21, 2025 katika Hoteli ya Midland Jijini Dodoma huku yakihusisha uwasilishaji wa mada na majadiliano, pamoja na maswali na majibu ya papo kwa papo.

Aidha mafunzo hayo yalilenga kuhakikisha Taasisi zote za umma na Mamlaka za Serikali za mitaa zinahakikisha matakwa ya Sheria ya Usimamizi wa Mazingira ya mwaka 2004 na Kanuni zake yanatekelezwa ipasavyo


Afisa Mazingira Mkuu wa NEMC na Mratibu Mkuu wa Mradi wa EMA upande wa NEMC, Bw. Paul Mashaija Kalokola akizungumza katika Mafunzo hiyo

Baadhi ya mada zilizowasilishwa ni pamoja na hali ya udhibiti wa taka za kielekroniki katika miji na manispaa, changamoto na fursa zilizopo katika taka za kielektroniki,  Udhibiti wa madampo haramu, Mpango mkakati wa Tathmini ya Athari kwa Mazingira, Mchakato wa Tathmini ya Athari kwa Mazingira na Jamii pamoja na Kaguzi za Mazingira pamoja na mchakato wa kupata vibali vya taka hatarishi pamoja na changamoto zilizopo katika udhibiti wake. 


Baadhi ya maafisa wa NEMC wakiwasilisha mada katika Mafunzo hiyo

Katika kuhitimisha mafunzo hayo baadhi ya washiriki wamelishukuru Baraza kwa mafunzo hayo huku wakieleza kuwa wamepata mbinu mpya ambazo awali hawakuwa nazo katika swala zima la Usimamizi wa Mazingira nchini.



Baadhi ya washiriki wa Semina hiyo

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni

NEMC YASHIRIKI MKUTANO WA SABA WA UMOJA WA MATAIFA KUHUSU MAZINGIRA

Baraza la Taifa la Hifadhi na Usimamizi wa Mazingira (NEMC) linashiriki Mkutano wa Saba (07) wa Umoja wa Mataifa kuhusu Mazingira (07th Unit...