Nyumbani

𝐁𝐎𝐃𝐈 𝐘𝐀 𝐍𝐄𝐌𝐂 𝐘𝐀𝐍𝐎𝐋𝐄𝐖𝐀 𝐌𝐅𝐔𝐌𝐎 𝐖𝐀 𝐔𝐅𝐔𝐀𝐓𝐈𝐋𝐈𝐀𝐉𝐈 𝐌𝐀𝐙𝐈𝐍𝐆𝐈𝐑𝐀 𝐊𝐈𝐃𝐈𝐉𝐈𝐓𝐀𝐋𝐈


Bodi ya Wakurugenzi ya Baraza la Taifa la Hifadhi na Usimamizi wa Mazingira (NEMC) imepitishwa kwenye wasilisho maalum kuhusu Mfumo wa Kidijitali wa Kufuatilia Uchafuzi wa Mazingira ujulikanao kama Online Continuous Emissions Monitoring System (OCEMS).

Mfumo huu wa kisasa umeundwa kwa lengo la kufanikisha ufuatiliaji wa wakati halisi wa viwango vya uchafuzi vinavyotolewa na viwanda na sekta mbalimbali, hatua inayolenga kuongeza uwazi, uwajibikaji na ufanisi katika kusimamia mazingira nchini.

Kupitia mfumo huu, taarifa za uchafuzi wa hewa zitapatikana moja kwa moja na kwa wakati  jambo ambalo litasaidia katika kufanya uamuzi sahihi kuhusu hatua za kudhibiti uchafuzi. Aidha, mfumo huu utawezesha kuimarika kwa ushirikiano kati ya wadau wa mazingira kwa kuwa taarifa zitakuwa wazi na zinazopatikana kwa urahisi, hivyo kuchochea jitihada za pamoja katika kulinda mazingira na afya ya jamii.


Bodi ya NEMC ikipatiwa Mafunzo ya mfumo wa ufuatiliaji wa Mazingira Kidigitali

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni

NEMC YASHIRIKI MKUTANO WA SABA WA UMOJA WA MATAIFA KUHUSU MAZINGIRA

Baraza la Taifa la Hifadhi na Usimamizi wa Mazingira (NEMC) linashiriki Mkutano wa Saba (07) wa Umoja wa Mataifa kuhusu Mazingira (07th Unit...