Nyumbani

NEMC YAKAGUA MGODI WA 'URANIUM' MKOANI RUVUMA UNAOTARAJIWA KUANZA 2026

Baraza la Taifa la Hifadhi na Usimamizi wa Mazingira (NEMC) lilifika na kukagua Mgodi wa madini aina ya Uranium uliopo katika Wilaya ya Namtumbo Mkoani Ruvuma ambao ulikuwa katika Uchimbaji mdogo wa majaribio huku Uchimbaji mkubwa ukitarajiwa kuanza mwaka 2026.

NEMC ilifika na kufanya Ukaguzi katika Mgodi huo na kutekeleza majukumu yake ya kuhakikisha shughuli za Uchimbaji katika Mgodi huo haziathiri Mazingira, Viumbe hai na wakazi wa jirani na Mgodi huo ikiwa ni agizo la Serikali.

Awali NEMC ilianza kwa kutoa elimu ya Mazingira na Afya kwa wakazi wa vijiji vilivyo karibu na Mgodi huo ili kuwajengea uelewa kuhusiana na madini ya 'Uranium' jinsi yanavyoweza kuhatarisha afya na Mazingira ikiwa hayata chakatwa na kudhibitiwa kwa umakini.

Akizungumza katika Ukaguzi huo Kaimu Mkurugenzi wa Uzingatiaji na Utekelezaji wa Sheria Bw. Jamal Baruti alisema NEMC ilifika katika Mgodi huo kufanya Ukaguzi ili kutathmini ikiwa wawekezaji katika Mgodi huo wamekidhi na kuzingatia miondombinu ya Mazingira ambayo haita haribu Mazingira, kuhatarisha usalama wa wakazi na wafanyakazi katika Mgodi huo kabla Uchimbaji mkubwa haujaanza.

Timu ya wataalamu wa Mazingira kutoka NEMC na Kampuni ya Uchimbaji ya MANTRA wakikagua moja ya mlima wenye madini ya  'Urunium' wakati wa ukaguzi wa Mgodi huo. Wa pili kulia ni Kaimu Mkurugenzi wa Uzingatiaji na Utekelezaji wa Sheria (NEMC) Bw. Jamal Baruti.

Aidha Bw. Baruti alieleza kuwa Mradi wa Mgodi huo utakuwa na uwezo wa kuzalisha tani elfu 27 kwa siku na utakuwa ni Mradi mkubwa wa Uchimbaji madini nchini ukilinganisha na Miradi mingine nchini Tanzania.

Aliongeza kuwa Tanzania  itakuwa nchi ya nne ya uzalishaji wa madini ya 'Uranium' Duniani huku akiwasisitiza wawekezaji na wananchi kuzingatia uhifadhi Mazingira na si tu kuangalia manufaa ya Mgodi huo.

Meneja wa Kampuni ya MANTRA Bw. Beria Vorster akitoa maelezo kwa wataalamu wa Mazingira kutoka NEMC wakati wa ukaguzi wa mtambo wa kuchenjua madini ya 'Urunium' ikiwa ni sehemu ya Ukaguzi wa Mgodi huo.

Kwa upande wake Meneja Kanda ya Kusini (NEMC) Bw. Boniface Guni alisema ziara hiyo iliwasaidia NEMC kupata picha ya Mradi huo ambayo itawasaidia kusimamia Mpango wa Usimamizi wa Mazingira na jamii ipasavyo.

Naye Mwenyekiti wa Kitongoji cha Buchushu Kijiji cha Iguseka Bw. Omary Rashid aliishukuru NEMC kwa kuwapatia elimu hiyo adhimu ya Mazingira wakazi wa vijiji hivyo ambayo ni muhimu katika utunzaji wa Mazingira na Afya ya binadamu.

Timu ya wataalamu wa Mazingira kutoka NEMC na Kampuni ya Uchimbaji ya MANTRA wakiwa katika picha ya pamoja mara baada ya ukaguzi wa Mgodi wa madini ya 'Urunium' katika eneo la Mto Mkuju Wilayani Namtumbo Mkoani Ruvuma. Wa katikati ni Kaimu Mkurugenzi wa Uzingatiaji na Utekelezaji wa Sheria NEMC Bw. Jamal Baruti na kushoto kwake ni Meneja wa Mradi Bw. Beria Vorster

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni

NEMC YASHIRIKI MKUTANO WA SABA WA UMOJA WA MATAIFA KUHUSU MAZINGIRA

Baraza la Taifa la Hifadhi na Usimamizi wa Mazingira (NEMC) linashiriki Mkutano wa Saba (07) wa Umoja wa Mataifa kuhusu Mazingira (07th Unit...