Nyumbani

RUVUMA YAFIKIWA ELIMU YA MAZINGIRA- MADINI YA URANIUM

Baraza la Taifa la Hifadhi na Usimamizi wa Mazingira (NEMC) lilitoa elimu ya kimazingira na afya kwa vijiji viwili vya Mtonya na Mandela-Likuyu katika Halmashauri ya Wilaya ya Namtumbo Mkoani Ruvuma kufuatia Mradi wa Uchimbaji wa Madini aina ya 'Uranium'  ulitarajiwa kuanza katika mgodi ulio karibu na vijiji hivyo.

Elimu hiyo ilitolewa kwa wananchi kuanzia 8-9 Septemba, 2025 kwa vijiji hivyo huku ikifuatiwa na ukaguzi uliofanyika katika mgodi huo ambapo ilikuwa hatua ya awali ya kuelimisha jamii na wawekezaji kabla ya Mradi huo kuanza ambapo  ni maagizo yaliyotolewa na Serikali ili kuhakikisha jamii inatambua uwepo wa Mradi huo na kuhakikisha  jamii haiathiriki na Mradi huo.

Mkurugenzi wa Uzingatiaji na Utekelezaji wa Sheria (NEMC) Bw. Jamal Baruti akizungumza wakati wa utoaji wa elimu ya ya Mazingira na Afya kwa wanakijiji wa Mtonya Wilayani Namtumbo Mkoani Ruvuma kufuatia Uchimbaji mkubwa wa madini ya 'Urunium' utakaoanza mwakani 2026

Meneja Kanda ya Kusini NEMC Bw. Boniface Guni akiwasilisha mada kwa wanakijiji wa Mandela-Likuyu Wilayani Namtumbo Mkoani Ruvuma wakati wa utoaji wa elimu ya Mazingira na Afya kufuatia Uchimbaji mkubwa wa madini ya 'Urunium' utakaoanza mwakani 2026

Meneja Kanda ya Kusini NEMC Bw. Boniface Guni akiwasilisha mada kwa wanakijiji wa Mtonya Wilayani Namtumbo Mkoani Ruvuma wakati wa utoaji wa elimu ya Mazingira na Afya kufuatia Uchimbaji mkubwa wa madini ya 'Urunium' utakaoanza mwakani 2026

Akizungumza katika utoaji wa elimu hiyo kwa niaba ya Mkurugenzi Mkuu wa NEMC Dkt. Immaculate Sware Semesi, Kaimu Mkurugenzi wa Uzingatiaji na Utekelezaji wa Sheria (NEMC) Bw. Jamal Baruti aliutaka Uongozi wa vijiji hivyo kutumia Kamati za Mazingira na kushirikiana na Serikali kuendelea kuelimisha jamii juu ya maswala ya Mazingira na Afya ya jamii yanayoweza kusababishwa na Mradi huo.

Kwa upande wake, Meneja Kanda ya Kusini (NEMC) Bw. Boniface Guni aliwataka wakazi wa vijiji hivyo kuchangamkia fursa za ajira katika Mradi huo huku wakizingatia ulinzi wa Afya zao na Mazingira.

Aidha Kaimu Mkurugenzi wa Uzingatiaji na Utekelezaji wa Sheria NEMC Bw. Jamal Baruti alisema NEMC itaendelea na ufuatiliaji wa maswala ya kimazingira kwa kushirikiana na Taasisi nyingine huku akiitaka Kampuni ya Mantra TZ LTD ya Uchimbaji katika mgodi huo kutambua haki za wakazi wa vijiji hivyo na kuchangia shughuli za maendeleo ya wakazi wa vijiji hivyo kama manufaa ya Mradi huo.

Mkurugenzi wa Uzingatiaji na Utekelezaji wa Sheria (NEMC) Bw. Jamal Baruti (wa tatu kulia waliokaa) akiwa katika picha ya pamoja na baadhi ya wanakijiji na Viongozi wa Kijiji cha Mtonya Wilayani Namtumbo Mkoani Ruvuma mara baada ya kuwapatia elimu ya Mazingira na Afya kufuatia Uchimbaji mkubwa wa madini ya 'Urunium' utakaoanza mwakani 2026

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni

NEMC YASHIRIKI MKUTANO WA SABA WA UMOJA WA MATAIFA KUHUSU MAZINGIRA

Baraza la Taifa la Hifadhi na Usimamizi wa Mazingira (NEMC) linashiriki Mkutano wa Saba (07) wa Umoja wa Mataifa kuhusu Mazingira (07th Unit...