Baraza la Taifa la Hifadhi na Usimamizi wa Mazingira (NEMC) linashiriki Maonesho ya Kimataifa ya Biashara na Uwekezaji Kusini (Kusini International Trade Fair and Festival) yanayofanyika kuanzia tarehe 14-21, Septemba, 2025 katika eneo la fukwe ya Matema Wilaya ya Kyela Mkoani Mbeya.
Maonesho hayo yamelenga kutangaza fursa za kibiashara zilizopo katika mikoa ya Kusini ambapo NEMC inatumia fursa hiyo kutoa elimu ya Mazingira.
Maafisa Mazingira wa NEMC Kanda ya Kusini wakitoa elimu kwa wananchi waliotembelea banda lao katika maonesho hayo.
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni