Nyumbani

WAHANDISI WA NEMC WASHIRIKI MAADHIMISHO YA 22 YA SIKU YA WAHANDISI NCHINI (22ND AED 2025)

Wahandisi wa Baraza la Taifa la Hifadhi na Usimamizi wa Mazingira (NEMC) wanashiriki Maadhimisho ya 22 ya Siku ya Wahandisi nchini (AED 2025) yanayofanyika Ukumbi wa Mlimani City, Dar es Salaam kuanzia tarehe 24 - 26 Septemba, 2025 chini ya kauli mbiu isemayo "Kufanikisha Dira ya 2025 na Kusonga Mbele kuelekea Dira ya 2050: Nafasi ya Wahandisi."

Tukio hili limewaleta pamoja wahandisi zaidi ya 4,000, watunga sera, na wadau mbalimbali kujadili masuala muhimu ikiwemo maadili katika uhandisi, mabadiliko ya kidijitali, miundombinu ya kijani, nishati, maji, kilimo, ushindani wa viwanda, na maendeleo endelevu.

Kupitia ushiriki huu, wahandisi wa NEMC wanaendelea kuimarisha nafasi yao katika kuunganisha ubunifu wa uhandisi na uwajibikaji katika kusimamia uhifadhi wa mazingira ili kuhakikisha kwamba safari ya Tanzania kuelekea Dira ya 2050 inabaki endelevu, jumuishi, na yenye ustahimilivu.


Wahandisi wa Mazingira (NEMC) wakiwa katika picha ya pamoja nje ya Ukumbi wa Mlimani City Jijini Dar es salaam  wakati wa Maadhimisho ya 22 ya Siku ya Wahandisi nchini 

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni

NEMC YASHIRIKI MKUTANO WA SABA WA UMOJA WA MATAIFA KUHUSU MAZINGIRA

Baraza la Taifa la Hifadhi na Usimamizi wa Mazingira (NEMC) linashiriki Mkutano wa Saba (07) wa Umoja wa Mataifa kuhusu Mazingira (07th Unit...