Baraza la Taifa la Hifadhi na Usimamizi wa Mazingira (NEMC) limeshiriki Kongamano la Dunia la Programu ya UNESCO ya Binadamu na Hifadhi Hai lililofanyika Jijini Hangzhou nchini China kuanzia tarehe 22-25 Septemba 2025.
Kwa upande wa NEMC Kongamano hilo limehudhuriwa na Mkurugenzi Mkuu wa Baraza Dkt. Immaculate Sware Semesi pamoja na Meneja wa Tafiti za Mazingira (NEMC) Dkt. Rose Sallema.
Wawakilishi wengine kutoka Tanzania katika kongamano hilo ni kutoka TANAPA
Kongamano hilo limelenga Kuimarisha ushirikiano wa Kimataifa, kupata maarifa na teknolojia mpya katika kusimamia na kuhifadhi Mazingira nchini, ni fursa katika uendelevu wa Hifadhi za Taifa, fursa za Kutangaza vivutio vya kitalii, kuimarisha Ushirikiano na Jamii, kuitangaza Tanzania kimataifa, kuvutia wawekezaji na kusaidia kufikia malengo ya Maendeleo nchini.
Mkurugenzi Mkuu wa NEMC Dkt. Immaculate Sware Semesi (wa pili kushoto) katika Ukumbi wa Kongamano hilo, kushoto kwake ni Meneja Tafiti za Mazingira (NEMC) Dkt. Rose Sallema pamoja na washiriki wengine wa Kongamano hilo lililofanyika Nchini China
Meneja Tafiti za Mazingira (NEMC) Dkt. Rose Sallema (wa katikati) na baadhi ya washiriki wa Kongamano hilo.
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni