Nyumbani

𝐍𝐄𝐌𝐂 𝐘𝐀𝐄𝐍𝐃𝐄𝐒𝐇𝐀 𝐌𝐀𝐅𝐔𝐍𝐙𝐎 𝐘𝐀 𝐍𝐃𝐀𝐍𝐈 𝐉𝐔𝐔 𝐘𝐀 𝐌𝐀𝐏𝐈𝐓𝐈𝐎 𝐘𝐀 𝐓𝐀𝐀𝐑𝐈𝐅𝐀 𝐙𝐀 𝐓𝐀𝐓𝐇𝐌𝐈𝐍𝐈 𝐘𝐀 𝐀𝐓𝐇𝐀𝐑𝐈 𝐊𝐖𝐀 𝐌𝐀𝐙𝐈𝐍𝐆𝐈𝐑𝐀 𝐍𝐀 𝐉𝐀𝐌𝐈𝐈 𝐍𝐀 𝐊𝐀𝐆𝐔𝐙𝐈 𝐙𝐀 𝐌𝐀𝐙𝐈𝐍𝐆𝐈𝐑𝐀

Baraza la Taifa la Hifadhi na Usimamizi wa Mazingira (NEMC) kupitia Kurugenzi ya Tathmini ya Athari kwa Mazingira na Jamii limeendelea kujenga uwezo kwa watumishi wake kwa kuendesha mafunzo ya ndani yahusuyo mapitio ya taarifa za Tathmini ya Athari kwa Mazingira na Jamii (TAM) pamoja na kaguzi za mazingira. 

Mafunzo hayo ya siku nne yalifanyika kuanzia tarehe 18 hadi 21 Novemba 2025 yakilenga kuongeza weledi na kuimarisha utendaji katika kupitia taarifa na kufanya kaguzi za miradi inayowasilishwa kwa Baraza, kuimarisha umahiri wa watumishi hao na kuandaa timu madhubuti yenye uwezo wa kushughulikia kwa haraka na kwa ubora wa juu taarifa za tathmini na kaguzi za mazingira zinazowasilishwa na wawekezaji kwa Baraza.

Mkurugenzi wa Tathmini ya Athari kwa Mazingira na Jamii (NEMC) Bi. Lilian Lukambuzi akiwasilisha mada katika mafunzo hayo
Mafunzo haya yalifunguliwa rasmi na Mkurugenzi wa Tathmini ya Athari kwa Mazingira na Jamii, Bi. Lilian Lukambuzi, na kuendeshwa na wataalamu kutoka ndani ya Kurugenzi hiyo wakiwemo Eng. Luhuvilo Mwamila "Kaimu Meneja Mapitio ya Tathmini ya Athari kwa Mazingira na Jamii" na Bi. Edika Masisi "Meneja Usajili wa Wataalamu Elekezi wa Mazingira". Washiriki walipata nafasi ya kujifunza kwa undani namna bora za kufanya mapitio ya taarifa za TAM, vigezo vya tathmini, na hatua muhimu katika ukaguzi wa mazingira ili kuhakikisha miradi inazingatia sheria ya Mazingira.

Aidha, mafunzo hayo yaliwalenga watumishi wa NEMC kutoka kanda za Mashariki Kaskazini, Mashariki Kusini, Ilala, Temeke, Bagamoyo pamoja na Makao Makuu.














Hakuna maoni:

Chapisha Maoni

NEMC YASHIRIKI MKUTANO WA SABA WA UMOJA WA MATAIFA KUHUSU MAZINGIRA

Baraza la Taifa la Hifadhi na Usimamizi wa Mazingira (NEMC) linashiriki Mkutano wa Saba (07) wa Umoja wa Mataifa kuhusu Mazingira (07th Unit...