Nyumbani

𝐍𝐄𝐌𝐂 𝐘𝐀𝐄𝐍𝐃𝐄𝐒𝐇𝐀 𝐌𝐀𝐅𝐔𝐍𝐙𝐎 𝐊𝐔𝐇𝐔𝐒𝐔 𝐍𝐘𝐄𝐍𝐙𝐎 𝐙𝐀 𝐔𝐒𝐈𝐌𝐀𝐌𝐈𝐙𝐈 𝐖𝐀 𝐌𝐀𝐙𝐈𝐍𝐆𝐈𝐑𝐀 𝐊𝐖𝐀 𝐖𝐈𝐙𝐀𝐑𝐀, 𝐓𝐀𝐀𝐒𝐈𝐒𝐈 𝐍𝐀 𝐇𝐀𝐋𝐌𝐀𝐒𝐇𝐀𝐔𝐑𝐈 𝐙𝐀 𝐌𝐀𝐍𝐈𝐒𝐏𝐀𝐀 𝐍𝐀 𝐖𝐈𝐋𝐀𝐘𝐀

Baraza la Taifa la Hifadhi na Usimamizi wa Mazingira (NEMC) linaendeaha mafunzo kuhusu nyenzo za usimamizi wa mazingira kwa Wizara, Taasisi pamoja na Halmashauri za Manispaa na Wilaya nchini. Mafunzo haya yameandaliwa kupitia Mradi wa kujenga uwezo wa kitaifa katika kusimamia Sheria ya usimamizi wa Mazingira ya mwaka 2004. Mradi huu unafadhiliwa na Shirika la Maendeleo la Sweden (SIDA). Mradi unalenga kuimarisha uelewa na uwezo wa watumishi katika kusimamia Sheria ya mazingira kwa ufanisi katika utekelezaji wa majukumu katika maeneo yao ya kazi.


Mafunzo hayo ya siku mbili yameanza tarehe 27 na kumalizika 28 Novemba 2025 jijini Dodoma. Kupitia mafunzo haya, washiriki wanapata maarifa ya kutathmini athari za kimazingira pamoja na kupanga mikakati endelevu ya utunzaji wa mazingira huku wakizingatia Nguzo ya tatu ya Dira ya maendeleo ya Taifa 2050 ambayo imeweka mkazo juu ya kuzingatia masuala ya utunzaji wa Mazingira nchini.

Akifungua mafunzo hayo, Meneja wa maeneo maalum na mabadiliko ya tabianchi kutoka NEMC, Dkt. Careen Kahangwa, aliwataka washiriki kutumia fursa hiyo kuboresha utendaji katika maeneo yao ya kazi. Mafunzo haya yanaendeshwa na timu ya wataalamu kutoka NEMC. Aidha wataalamu kutoka Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG), Ofisi ya Makamu wa Rais na taasisi binafsi ya Taka ni ajira nao walishiriki Katika kutoa mafunzo.

Washiriki wa mafunzo hayo wamepata nafasi ya kujadili kwa kina changamoto za kimazingira zinazojitokeza katika taasisi zao na kujifunza mbinu bora za kukabiliana nazo. Kupitia mafunzo haya, wanatarajiwa kuboresha mifumo ya ufuatiliaji, utoaji taarifa, na utekelezaji wa sheria na kanuni za mazingira nchini. Hatua hii muhimu itachangia kwa kiasi kikubwa kulinda na kuhifadhi mazingira kwa manufaa ya kizazi cha sasa na kijacho.







Hakuna maoni:

Chapisha Maoni

NEMC YASHIRIKI MKUTANO WA SABA WA UMOJA WA MATAIFA KUHUSU MAZINGIRA

Baraza la Taifa la Hifadhi na Usimamizi wa Mazingira (NEMC) linashiriki Mkutano wa Saba (07) wa Umoja wa Mataifa kuhusu Mazingira (07th Unit...