Nyumbani

NEMC YASHIRIKI KIKAO KAZI CHA KUPITIA MPANGO WA KITAIFA WA KUPAMBANA NA UKAME

Baraza la Taifa la Hifadhi na Usimamizi wa Mazingira (NEMC) limeshiriki kikao kazi cha kupitia Mpango wa Kitaifa wa kupambana na ukame kilichofanyika katika Chuo Kikuu cha Sokoine cha Kilimo (SUA), mkoani Morogoro.
Akizungumza katika kikao hicho, muwakilishi kutoka NEMC ambaye pia ni Afisa Mazingira Mkuu Bi.Marlene Moshi amesema ushiriki wa NEMC ni muhimu katika kuhakikisha kuwa mikakati ya kitaifa inakwenda sambamba na malengo ya kimataifa ya kupunguza athari za ukame na kulinda mazingira.

Kikao hicho kimeratibiwa na Ofisi ya Makamu wa Rais (VPO) kupitia Idara ya Mazingira, kikilenga kuhakikisha utekelezaji wa Mpango wa Umoja wa Mataifa wa Kupambana na Kuenea kwa Jangwa na Ukame Duniani.


Hakuna maoni:

Chapisha Maoni

NEMC YASHIRIKI MKUTANO WA SABA WA UMOJA WA MATAIFA KUHUSU MAZINGIRA

Baraza la Taifa la Hifadhi na Usimamizi wa Mazingira (NEMC) linashiriki Mkutano wa Saba (07) wa Umoja wa Mataifa kuhusu Mazingira (07th Unit...