Nyumbani

NEMC KANDA YA ILALA YAKUTANA NA UONGOZI WA BENKI YA EQUITY KUJADILI FURSA ZA MAZINGIRA

 

NEMC Kanda ya Ilala, imekutana na uongozi wa Benki ya Equity kwa lengo la kujadili fursa za mashirikiano zilizopo katika sekta ya mazingira pamoja na utoaji wa elimu ya fedha. 

Kikao hicho kilichofanyika Januari 04, 2026 katika ofisi za NEMC jijini Dar es Salaam, kimeongozwa na Kaimu Meneja wa NEMC Kanda ya Ilala, Bi. Abela Muyungi, na kuwahusisha Meneja wa Tawi la Equity–Nyerere Road pamoja na Meneja wa Mahusiano wa benki hiyo. Majadiliano hayo yamejikita katika utoaji wa elimu ya mazingira, matumizi ya nishati safi, uzingatiaji wa sheria na kanuni za mazingira katika viwanda, pamoja na huduma za kifedha.




Hakuna maoni:

Chapisha Maoni

TIMU YA UKAGUZI WA MAZINGIRA KUTOKA NEMC MAKAO MAKUU NA KANDA YA ZIWA VICTORIA MASHARIKI WAADHIMISHA MEIMOSI 2026 KWA KUPANDA MITI MAKUMBUSHO YA MWL. JULIUS K. NYERERE, BUTIAMA

Timu ya watumishi wa Baraza la Taifa la Hifadhi na Usimamizi wa Mazingira (NEMC) wanaofanya ukaguzi wa mazingira katika mikoa ya Kanda ya Zi...