NEMC Kanda ya Ilala, imekutana na uongozi wa Benki ya Equity kwa lengo la kujadili fursa za mashirikiano zilizopo katika sekta ya mazingira pamoja na utoaji wa elimu ya fedha.
Kikao hicho kilichofanyika Januari 04, 2026 katika ofisi za NEMC jijini Dar es Salaam, kimeongozwa na Kaimu Meneja wa NEMC Kanda ya Ilala, Bi. Abela Muyungi, na kuwahusisha Meneja wa Tawi la Equity–Nyerere Road pamoja na Meneja wa Mahusiano wa benki hiyo. Majadiliano hayo yamejikita katika utoaji wa elimu ya mazingira, matumizi ya nishati safi, uzingatiaji wa sheria na kanuni za mazingira katika viwanda, pamoja na huduma za kifedha.
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni