Nyumbani

DKT. MKAMA AZURU BANDA LA NEMC MAONESHO YA KUELEKEA SIKU YA MAZINGIRA DUNIANI JUNI 5

Naibu Waziri wa Mawasiliano na Teknolojia ya Habari Dkt. Switbert Zacharia Mkama (Mb)

ametembelea Banda la NEMC katika maonesho ya Maadhimisho ya wiki ya Mazingira Duniani yanayofanyika katika viwanja vya Jakaya Kikwete (JKCC) jijini Dodoma.

Aidha, Mhe. Naibu Waziri alipozungumza, ameitaka NEMC kuongeza nguvu katika udhibiti wa maswala ya uharibifu wa Mazingira ikiwa ni pamoja na uchomaji holela wa misitu. Pia kutoa elimu kwa makundi yote ya jamii kuanzia vijana mpaka wazee, ufuatiliaji wa misitu kupitia Kanda za NEMC, kutoa elimu kwa jamii kuhusu umuhimu wa kutunza vyanzo vya maji na kuhimiza usafi kwa mito inayokabiliwa na uchafuzi.









Hakuna maoni:

Chapisha Maoni

𝗡𝗘𝗠𝗖 𝗬𝗔𝗞𝗨𝗧𝗔𝗡𝗔 𝗡𝗔 𝗪𝗔𝗔𝗡𝗗𝗔𝗔𝗝𝗜 𝗪𝗔 𝗧𝗔𝗡𝗭𝗔𝗡𝗜𝗔 𝗚𝗥𝗘𝗘𝗡 𝗦𝗨𝗠𝗠𝗜𝗧 𝟮𝟬𝟮𝟲

Baraza la Taifa la Hifadhi na Usimamizi wa Mazingira (NEMC) limekutana na ujumbe wa waandaaji wa Tanzania Green Summit (TGS), inayotarajiwa ...