Baraza la Taifa la Hifadhi na Usimamizi wa Mazingira (NEMC) leo 22 Agosti, 2025 limeshiriki Kongamano la Pika Kijanja lililoandaliwa na TBC pamoja na Bongo FM ambalo ni sehemu ya Kampeni ya kuhamasisha matumizi ya Nishati safi ya kupikia.
Kongamano hilo limefanyika katika Ukumbi wa Ubungo plaza ambapo mgeni rasmi alikuwa ni Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam Mhe. Albert Chalamila.
Akizungumza, mgeni katika Kongamano hilo, Mkuu wa Mkoa wa Dar es salaam mhe. Albert Chalamila, amesema jamii ikiendelea kutumia nishati chafu ya kupikia itahatarisha usalama wa vizazi vijavyo kutokana na uharibifu wa mazingira unaosababishwa na matumizi ya nishati hiyo, jambo ambalo ameliita ni usaliti wa dunia ijayo.
Katika Kongamano hilo NEMC pia imeshiriki majadiliano yaliyolenga kuelimisha na kuhamasisha jamii juu ya umuhimu wa matumizi ya Nishati safi ya kupitia ikiwemo gesi na pia kuelimisha kuhusu madhara ya Nishati chafuzi kwa Afya na Mazingira.
Baadhi ya Maafisa wa NEMC katika Kongamano hiloKongamano hili lililowakutanisha wadau mbalimbali wa Nishati na Mazingira wakiwemo wanawake linafanyika kwa mara ya tano tangu kampeni ya Pika Kijanja ilipoanzishwa mwaka 2022
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni