Nyumbani

NEMC YASHIRIKI UKAGUZI WA BWAWA LA TOPESUMU ZAMBIA

Wataalam wa miamba na madini kutoka Baraza la Taifa la Hifadhi na Usimamizi wa Mazingira (NEMC) Bw. Abel Sembeka na Bi. Edika Masisi, wameshiriki katika warsha na ukaguzi wa bwawa la topesumu lililopasuka Februari 15, 2025 kwenye mgodi wa kampuni ya Sino Metal Leach Zambia Limited nchini Zambia.

Warsha hiyo imeandaliwa na Taasisi ya Jiolojia ya Sweden (SGU) kwa kushirikiana na Chuo Kikuu cha Teknolojia cha Lulea kutoka nchini Sweden na Chuo Kikuu cha Copperbelt cha nchini Zambia, huku Wizara ya Madini na Mamlaka ya Usimamizi wa Mazingira nchini Zambia (ZEMA) wakiwa wenyeji.

Warsha hiyo umehusisha pia wataalam wa migodi na mazingira kutoka nchi za Afrika Magharibi, Mashariki na Kusini mwa Afrika waliopata mafunzo ya usimamizi wa miamba taka na maji migodini kupitia mradi wa ITP 308 chini ya uratibu wa SGU.

Lengo kuu la warsha hiyo ni kutembelea na kufanya tathmini ya bwawa la topesumu lililopasuka, kujifunza chanzo cha tatizo, mbinu bora za usanifu na usimamizi wa mabwawa ya topesumu, pamoja na hatua za kupunguza madhara kwa mazingira na jamii zinazozunguka maeneo ya migodi.






Hakuna maoni:

Chapisha Maoni

NEMC YASHIRIKI MKUTANO WA SABA WA UMOJA WA MATAIFA KUHUSU MAZINGIRA

Baraza la Taifa la Hifadhi na Usimamizi wa Mazingira (NEMC) linashiriki Mkutano wa Saba (07) wa Umoja wa Mataifa kuhusu Mazingira (07th Unit...