Baraza la Taifa la Hifadhi na Usimamizi wa Mazingira (NEMC) kupitia ofisi yake ya Kanda ya Nyanda za Juu Kusini wametoa Mafunzo ya Uhifadhi na Usimamizi wa Mazingira kwa Viongozi na Kamati za Mazingira za Wanawake na Samia katika Mkoa wa Njombe.
Mafunzo hayo yamelenga kupata Wadau na Mabalozi wazuri watakao saidia kusimamia, kutunza na kuelimisha wananchi na jamii kwa ujumla maswala ya Uhifadhi na Usimamizi wa Mazingira katika Mkoa wa Njombe
Elimu iliyotolewa ni pamoja na Umuhimu wa kutunza Mazingira na faida zake, Umuhimu wa Kutumia Nishati safi ya Kupikia na faida zake.
Kupitia mafunzo hayo, NEMC imewafahamisha washiriki wa mafunzo changamoto nane za kimazingira zilizoainishwa katika Sera ya Taifa ya Hifadhi na Usimamizi wa Mazingira ya Mwaka 2021 ambazo ni pamoja na Mabadiliko ya Tabianchi, Uharibifu wa Ardhi, Uharibifu wa Misitu, Uharibifu wa Vyanzo vya Maji na kupelekea uhaba na maji yenye ubora mijini na vijijini.
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni