Nyumbani

NEMC KANDA YA NYANDA ZA JUU KUSINI YAENDESHA MAFUNZO YA UHIFADHI NA USIMAMIZI WA MAZINGIRA, NJOMBE

Baraza la Taifa la Hifadhi na Usimamizi wa Mazingira (NEMC) kupitia ofisi yake ya Kanda ya Nyanda za Juu Kusini wametoa Mafunzo ya Uhifadhi na Usimamizi wa Mazingira kwa Viongozi na Kamati za Mazingira za Wanawake na Samia katika Mkoa wa Njombe.  

   

Mafunzo hayo yamelenga kupata Wadau na Mabalozi wazuri watakao saidia kusimamia, kutunza na kuelimisha wananchi na jamii kwa ujumla maswala ya Uhifadhi na Usimamizi wa Mazingira katika Mkoa wa Njombe 

Elimu iliyotolewa ni pamoja na Umuhimu wa kutunza Mazingira na faida zake, Umuhimu wa Kutumia Nishati safi ya Kupikia na faida zake.

Kupitia mafunzo hayo, NEMC imewafahamisha washiriki wa mafunzo changamoto nane za kimazingira zilizoainishwa katika Sera ya Taifa ya Hifadhi na Usimamizi wa Mazingira ya Mwaka 2021 ambazo ni pamoja na Mabadiliko ya Tabianchi,  Uharibifu wa Ardhi, Uharibifu wa Misitu, Uharibifu wa Vyanzo vya Maji na kupelekea uhaba na maji yenye ubora mijini na vijijini.

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni

TIMU YA UKAGUZI WA MAZINGIRA KUTOKA NEMC MAKAO MAKUU NA KANDA YA ZIWA VICTORIA MASHARIKI WAADHIMISHA MEIMOSI 2026 KWA KUPANDA MITI MAKUMBUSHO YA MWL. JULIUS K. NYERERE, BUTIAMA

Timu ya watumishi wa Baraza la Taifa la Hifadhi na Usimamizi wa Mazingira (NEMC) wanaofanya ukaguzi wa mazingira katika mikoa ya Kanda ya Zi...