Baraza la Taifa la Hifadhi na Usimamizi wa Mazingira (NEMC) limeshiriki semina kuhusu Mipango na Mikakati ya Serikali juu ya Uhifadhi na Usimamizi wa Mazingira iliyotolewa na Ofisi ya Makamu wa Rais kwa Kamati ya kudumu ya Bunge ya Maji na Mazingira iliyofanyika jijini Dodoma Februari 13, 2026.
Kwa upande wa NEMC, Semina hiyo imehudhuriwa na Mkurugenzi Mkuu wa NEMC, Dkt. Immaculate Sware Semesi ikiwa ni hatua mojawapo ya kuimarisha utekelezaji wa Mipango na Mikakati ya Uhifadhi na Usimamizi wa Mazingira nchini kama ilivyoainishwa katika Dira ya Taifa ya Maendeleo 2050.
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni