Baraza la Taifa la Hifadhi na Usimamizi wa Mazingira (NEMC) limeshiriki kikamilifu katika mkutano wa kusikiliza kero na malalamiko ya wananchi wa Wilaya ya Kinondoni, uliofanyika katika viwanja vya Nyakasangwe.
Mkutano huo umeandaliwa na Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam na kuhudhuriwa na viongozi mbalimbali wa serikali, wakiwemo Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Mheshimiwa Albert Chalamila, pamoja na Mkuu wa wilaya na viongozi wa Tasisi za Umma na wananchi wa Manispaa ya kinondoni
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni