Nyumbani

𝗡𝗘𝗠𝗖 𝗬𝗔𝗢𝗡𝗚𝗢𝗭𝗔 𝗠𝗔𝗝𝗔𝗗𝗜𝗟𝗜𝗔𝗡𝗢- 𝗪𝗔𝗥𝗦𝗛𝗔 𝗬𝗔 𝗞𝗜𝗞𝗔𝗡𝗗𝗔 𝗞𝗔𝗧𝗜 𝗬𝗔𝗞𝗘 𝗡𝗔 𝗖𝗦𝗘 𝗡𝗔 𝗜𝗡𝗗𝗜𝗔



 𝗡𝗶 𝗞𝗮𝘁𝗶𝗸𝗮 𝗙𝘂𝗿𝘀𝗮 𝘇𝗶𝗹𝗶𝘇𝗼𝗽𝗼 𝗸𝘄𝗲𝗻𝘆𝗲 𝗨𝘀𝗶𝗺𝗮𝗺𝗶𝘇𝗶 𝘄𝗮 𝘁𝗮𝗸𝗮 𝘇𝗮 𝗠𝗮𝘁𝗮𝗶𝗿𝗶 𝗖𝗵𝗮𝗸𝗮𝘃𝘂

Baraza la Taifa la Hifadhi na Usimamizi wa Mazingira (NEMC) Machi 25, 2026, limeendelea kuongoza majadiliano katika siku ya pili ya warsha ya Kikanda kuchochea fursa mpya katika Usimamizi wa taka za matairi chakavu ambapo mawasilisho ya kanuni za Usimamizi wa matairi chakavu (End-of-Life Tyres – ELTs) katika nchi zinazotekeleza mfumo wa Extended Producer Responsibility (EPR) yalifanyika.

Aidha, wasilisho la kitaalamu kutoka kituo cha Afrika Kusini cha kukuza uzalishaji wa kijani kuhusu umuhimu wa usimamizi wa matairi chakavu katika kulinda mazingira, kuchochea uchumi wa kijani na kuunda ajira, huku washiriki kutoka Ghana wakishirikisha uzoefu wa matumizi mbadala ya matairi chakavu na mbinu za kuwaunganisha wakusanyaji wadogo katika mfumo rasmi.

Kadhalika, mwakilishi kutoka Much Asphalt - Afrika Kusini aliwasilisha kuhusu matumizi ya teknolojia za kisasa zinazotumia matairi chakavu katika ujenzi wa barabara kama njia ya kuongeza thamani ya taka na kuboresha uimara wa barabara.

Kupitia warsha hiyo, NEMC imeongeza uelewa wa kuhusu mbinu bora za kuthibiti taka zitokanazo na matairi chakavu na kukuza uchumi rejeleshi.

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni

𝗡𝗘𝗠𝗖 𝗬𝗔𝗢𝗡𝗚𝗢𝗭𝗔 𝗠𝗔𝗝𝗔𝗗𝗜𝗟𝗜𝗔𝗡𝗢- 𝗪𝗔𝗥𝗦𝗛𝗔 𝗬𝗔 𝗞𝗜𝗞𝗔𝗡𝗗𝗔 𝗞𝗔𝗧𝗜 𝗬𝗔𝗞𝗘 𝗡𝗔 𝗖𝗦𝗘 𝗡𝗔 𝗜𝗡𝗗𝗜𝗔

 𝗡𝗶 𝗞𝗮𝘁𝗶𝗸𝗮 𝗙𝘂𝗿𝘀𝗮 𝘇𝗶𝗹𝗶𝘇𝗼𝗽𝗼 𝗸𝘄𝗲𝗻𝘆𝗲 𝗨𝘀𝗶𝗺𝗮𝗺𝗶𝘇𝗶 𝘄𝗮 𝘁𝗮𝗸𝗮 𝘇𝗮 𝗠𝗮𝘁𝗮𝗶𝗿𝗶 𝗖𝗵𝗮𝗸𝗮𝘃𝘂 Baraza la Ta...