Baraza la Taifa la Hifadhi na Usimamizi wa Mazingira (NEMC), kwa kushirikiana na Kituo cha Sayansi na Mazingira - India (CSE) wameandaa warsha ya kikanda inayolenga kujadili changamoto na fursa zitokanazo na ongezeko la taka za matairi chakavu.
Warsha hiyo imewakutanisha washiriki kutoka mamlaka za usimamizi wa mazingira na wadau mbalimbali kutoka nchi za Kenya, Uganda, Afrika Kusini, Ghana na Nigeria. Mkutano huu umefanyika katika Hoteli ya Four Points by Sheraton na New Africa Hotel jijini Dar es Salaam tarehe 23 na 24 Machi 2026.
Katika warsha hiyo, mada mbalimbali zimejadiliwa ikiwemo miundo ya kisheria na kikanuni, teknolojia za kuongeza thamani ya taka za matairi, pamoja na matumizi ya masoko katika kukuza dhana ya uchumi rejeleshi. Lengo kuu ni kubadilishana uzoefu na kubuni mbinu mbadala zitakazosaidia kupunguza athari za kimazingira huku zikichangia maendeleo endelevu ya kiuchumi katika ukanda wa Afrika.
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni