Baraza la Taifa la Hifadhi na Usimamizi wa Mazingira (NEMC), kwa kushirikiana na Shirika lisilo la kiserikali la kimataifa la WaterAid-Tanzania, limefanya ziara ya mafunzo nchini Rwanda. Mafunzo haya yameandaliwa na kutekelezwa na WaterAid-Rwanda, na yamefanyika katika Ofisi za shirika hilo.
Lengo kuu la mafunzo haya ni kujifunza namna WaterAid-Rwanda inavyotekeleza miradi ya maji, hususan katika eneo la Bugesera, ikiwa ni pamoja na mbinu za kuboresha upatikanaji wa maji safi na salama pamoja na usimamizi wa huduma za usafi wa mazingira.
Ziara hii ya mafunzo imehudhuriwa na viongozi na wataalamu mbalimbali, akiwemo Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Maji, Mkurugenzi Mkuu wa RUWASA, Mkurugenzi Msaidizi wa Usambazaji wa Maji na Usafi wa Mazingira, Afisa Tawala wa Mkoa wa Manyara, pamoja na maafisa wengine kutoka serikalini na WaterAid
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni