Nyumbani

NEMC KANDA YA ZIWA VICTORIA MASHARIKI YASHIRIKI ZIARA YA WAZIRI MASAUNI-MWANZA

Baraza la Taifa la Hifadhi na Usimamizi wa Mazingira (NEMC) limeshiriki ziara ya Waziri wa nchi, Ofisi ya Makamu wa Rais (Muungano na Mazingira) ya Ukaguzi wa Miradi ya uwekezaji Jijini Mwanza.

Ziara hiyo ililenga kukagua Miradi ya uwekezaji na namna inavyotekeleza Uhifadhi wa Mazingira Mkoani humo.

Akimpokea Mhe. Waziri katika Ofisi yake, Mkuu wa Mkoa wa Mwanza Mhe. Said Mtanda amesema Ofisi yake inafanya juhudi kubwa kushirikiana na  NEMC kuhakikisha Mazingira yanalindwa na kutunzwa katika Mkoa huo licha ya changamoto zinazoikabili Ofisi yake hasa katika udhibiti wa Kelele chafuzi za Maeneo ya kumbi za starehe.

Akizungumza na vyombo vya habari mara baada ya Ukaguzi huo, Mhe. Waziri amewataka wawekezaji na watanzania wote kulinda Mazingira huku akisisitiza kuwa Serikali haitasita kuwachukulia hatua wale wote wanaosababisha uharibifu wa Mazingira kwa namna yoyote.

"Tunawajibu wa kulinda Mazingira lli Mazingira yawe mazuri ni lazima sisi tuyalinde, na ili yawe mabaya ni lazima sisi tuyaharibu, Serikali inawajibu wa kuhakikisha watanzania wanaendelea kutunza Mazingira" amesema Mhe. Waziri Hamad Yusuf Masauni.



Hakuna maoni:

Chapisha Maoni

TIMU YA UKAGUZI WA MAZINGIRA KUTOKA NEMC MAKAO MAKUU NA KANDA YA ZIWA VICTORIA MASHARIKI WAADHIMISHA MEIMOSI 2026 KWA KUPANDA MITI MAKUMBUSHO YA MWL. JULIUS K. NYERERE, BUTIAMA

Timu ya watumishi wa Baraza la Taifa la Hifadhi na Usimamizi wa Mazingira (NEMC) wanaofanya ukaguzi wa mazingira katika mikoa ya Kanda ya Zi...