Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Mwigulu Nchemba akikabidhiwa Tuzo mnaalum na Waziri wa Nchi, Ofisi ya Makamu wa Rais (Muungano na Mazingira) Mhe. Mhandisi Hamad Yusuf Masauni ikiwa ni ishara ya kutambua mchango wake katika Uhifadhi na Usimamizi wa Mazingira nchini.
Tuzo hiyo ilikabidhiwa wakati wa Kongamano la Kisayansi lililoandaliwa na Baraza la Taifa la Hifadhi na Usimamizi wa Mazingira (NEMC) ikiwa ni sehemu ya Maadhimisho ya Miaka 40 ya NEMC lililofanyika katika Ukumbi wa Mikutano wa Julius Nyerere (JNICC), Jijini Dar es Salaam.
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni