Nyumbani

NEMC IKO KAZINI- ELIMU YA MAZINGIRA YAENDELEA KUTOLEWA VIWANJA VYA NANENANE - DODOMA

Baraza la Taifa la Hifadhi na Usimamizinw Mazingira (NEMC) limeendelea kuelimisha umma wa watanzania umuhimu wa kufanya kilimo, uvuvi na ufugaji salama unaozingatia misingi ya utunzaji Bora wa ardhi kwa maendeleo ya mazingira nchini.

Elimu hiyo inatolewa katika maonesho ya wakulima nanenane jijini Dodoma katika viwanja vya nzuguni yenye kaulimbiu isemayo " Chagua viongozi Bora kwa maendeleo endelevu ya kilimo, mifugo na uvuvi"


Timu ya NEMC ikiendelea na utoaji wa elimu ya Mazingira katika maonesho ya Wakulima, nanenane 2025 katika Viwanja vya Nzuguni jijini Dodoma 

NEMC inaendelea kuwakaribisha wadau wote wa Mazingira katika Banda lao lililopo viwanja vya Nanenane, nzuguni Dodoma, kwenye hema la tatu la Taasisi za Serikali ili kupata elimu ya mazingira kwa maendeleo endelevu ya kilimo, mifugo na uvuvi.



Wageni waliotembelea banda la NEMC katika maonesho nanenane 2025 wakisikiliza kwa makini elimu ya Mazingira inayotolewa na maafisa wa NEMC 


Hakuna maoni:

Chapisha Maoni

NEMC YASHIRIKI MKUTANO WA SABA WA UMOJA WA MATAIFA KUHUSU MAZINGIRA

Baraza la Taifa la Hifadhi na Usimamizi wa Mazingira (NEMC) linashiriki Mkutano wa Saba (07) wa Umoja wa Mataifa kuhusu Mazingira (07th Unit...