Nyumbani

NEMC YAPIGA KAMBI SABASABA – YAWAKARIBISHA WANANCHI KUPATA ELIMU YA MAZINGIRA

Baraza la Taifa la Hifadhi na Usimamizi wa Mazingira (NEMC) lilipiga kambi viwanja vya sabasaba maonesho ya 49 ya Biashara ya Kimataifa ili kutoa elimu ya uhifadhi na usimamizi wa mazingira kwa wananchi waliotembelea banda hilo katika Jengo la Karume.

Akizungumza katika maonesho hayo, Mhandisi Mwandamizi wa NEMC, Bw. Haji Kiselu, alisema Baraza limejipanga kikamilifu kuhakikisha elimu ya mazingira iliyo jumuishi inamfikia kila mwananchi, ili kwa pamoja tuweze kuyasimamia kwa maendeleo endelevu nchini.

Kwa upande wake, Mhandisi wa NEMC, Bw. Peres Ntinginya, alipozungumza, alisisitiza kuwa utunzaji wa mazingira ni jukumu la kila mmoja hivyo yapasa kuwajibika na kutoa  wito kwa wananchi kutumia nishati safi ya kupikia kwa kuwa matumizi yake husaidia kulinda afya ya binadamu na viumbe hai, kupunguza uzalishaji wa hewa ukaa, pamoja na kuhifadhi mazingira kwa ujumla.

Naye Mkazi wa Rufiji, Bw. Ayubu Njanja, alisema elimu aliyoipata kutoka kwa Maafisa wa Baraza imempa mwongozo sahihi wa kuzingatia katika kuhakikisha 

Bw. Ayubu Njanja akipatiwa elimu ya mazingira kutoka kwa wataalam wakati wa msimu wa maonesho ya 49 ya Sabasaba. 




Elimu ya Mazingira ikitolewa kwa wageni waliotembelea banda la NEMC katika  maonesho ya 49 ya Sabasaba 2025 




Elimu ya Mazingira ikitolewa kwa wageni waliotembelea banda la NEMC katika  maonesho ya 49 ya Sabasaba 2025 


Hakuna maoni:

Chapisha Maoni

NEMC YASHIRIKI MKUTANO WA SABA WA UMOJA WA MATAIFA KUHUSU MAZINGIRA

Baraza la Taifa la Hifadhi na Usimamizi wa Mazingira (NEMC) linashiriki Mkutano wa Saba (07) wa Umoja wa Mataifa kuhusu Mazingira (07th Unit...