Nyumbani

NEMC YAUNGANA NA TAASISI NYINGINE KUADHIMISHA SIKU MAALUMU YA MAZINGIRA MAONESHO YA SABASABA 2025

Baraza la Taifa la Hifadhi na Usimamizi wa Mazingira NEMC  Julai 6, 2025  limeungana na Taasisi mbalimbali kuadhimisha Siku ya maalumu ya Mazingira iliyotengwa kwa mara ya kwanza kwenye Maonesho ya Biashara ya Kimataifa (sabasaba) 2025.

Mgeni rasmi katika Maadhimisho hayo alikuwa ni Katibu Mkuu Ofisi ya Makamu wa Rais (Muungano na Mazingira) Mhandisi Cyprian Luhemeja huku tukio hilo likibebwa na Kauli mbiu isemayo "Matumizi ya Nishati safi na utunzaji wa Mazingira Kwa ustawi wa Tanzania bora".


Katibu Mkuu, Ofisi ya Makamu wa Rais, Mhandisi Cyprian Luhemeja akizungumza wakati wa hafla ya Siku maalumu ya Mazingira iliyotengwa katika maonesho ya Sabasaba 2025 iliyofanyika tarehe 6/7/2025

Akizungumza katika hotuba yake Mhe. Cyprian Luhemeja ameitaka siku hiyo ya tarehe 6 /7 itengwe rasmi kuwa siku maalumu ya Mazingira kila mwaka katika maonesho hayo kuanzia maonesho ya 50 ya biashara ya kimataifa (sabasaba).

Hafla ya Siku maalum ya Mazingira tarehe 6/7/2025 iliyotengwa katika msimu wa maonesho ya Sabasaba 2025

Sambamba na hilo amesisitiza watanzania wote kutunza Mazingira kwa kuwa Mazingira yaliumbwa kwanza Kisha mwanadamu akaumbwa baadae ili ayatunze, ayahifadhi na kuyalinda.

"Hii duniani ilianza kwa kutengenezewa Mazingira, mwanadamu ameumbwa wa mwisho baada ya Mazingira kutengenezewa na mwanadamu alipoumbwa alipewa kazi ya kuyatunza na kuyahifadhi Mazingira lakini mwanadamu anayaharibu kwa uchafuzi na ukataji wa miti.


Katibu Mkuu, Ofisi ya Makamu wa Rais Mhandisi Cyprian Luhemeja (wa nne kutoka kulia) akiwa katika picha ya pamoja na Mwenyekiti wa Bodi ya NEMC Bi. Mwanasha Tumbo (wa pili kulia) Mkurugenzi Mkuu wa NEMC Dkt. Immaculate Sware Semesi (wa tatu kushoto), Mkurugenzi Mkuu wa  Tantrade, Dkt. Latifa M. Khamis (wa tatu kulia), timu ya wanawake na Samia na baadhi ya washiriki wa Siku maalumu ya Mazingira iliyotengwa katika msimu wa maonesho ya Sabasaba 2025

Kwa upande wake Mkurugenzi Mkuu wa Baraza Dkt. Immaculate Sware Semesi amewapongeza washindi wa Mazingira Challenge iliyofanyika siku kadhaa zilizopita ambayo ililenga kumpata balozi kinara wa  Utunzaji wa Mazingira na anayehamasisha utunzaji wa Mazingira kwa kupiga picha ya Mazingira safi yanayomzunguka na kuwasilisha NEMC Kwa ajili ya mashindano hayo.

Maadhimisho hayo yalipambwa na mabalozi wa Mazingira pamoja na watumbuizaji nguli akiwemo Mrisho Mpoto pamoja na Mr. Tree na kuhudhuriwa na Viongozi mbalimbali akiwemo Mwenyekiti wa Bodi ya NEMC, Menejimenti ya NEMC, TANTRADE, STAMICO, Wanawake na Samia, Shirika la PUMA pamoja na wananchi waliotembelea maonesho ya sabasaba.


Katibu Mkuu, Ofisi ya Makamu wa Rais, Mhandisi Cyprian Luhemeja akimkabidhi zawadi na cheti cha heshima Mshindi wa kwanza wa mashindano ya ‘Mazingira Challenge’ Bw. Paulo Dotto Masele yaliyofanyika katika msimu wa sabasaba

Katibu Mkuu, Ofisi ya Makamu wa Rais, Mhandisi Cyprian Luhemeja akimkabidhi zawadi na cheti cha heshima Mshindi wa pili wa mashindano ya ‘Mazingira Challenge’ Bi. Magdalena Chuma yaliyofanyika katika msimu wa sabasaba


Katibu Mkuu, Ofisi ya Makamu wa Rais, Mhandisi Cyprian Luhemeja akimkabidhi zawadi na cheti cha heshima Mshindi wa tatu wa mashindano ya ‘Mazingira Challenge’ Bw. Stanley Urassa  yaliyofanyika katika msimu wa sabasaba

"Hii duniani ilianza kwa kutengenezewa Mazingira, mwanadamu ameumbwa wa mwisho baada ya Mazingira kutengenezewa na mwanadamu alipoumbwa alipewa kazi ya kuyatunza na kuyahifadhi Mazingira lakini mwanadamu anayaharibu kwa uchafuzi na ukataji wa miti.

Kwa upande wake Mkurugenzi Mkuu wa Baraza Dkt. Immaculate Sware Semesi amewapongeza washindi wa Mazingira Challenge iliyofanyika siku kadhaa zilizopita ambayo ililenga kumpata balozi kinara wa  Utunzaji wa Mazingira na anayehamasisha utunzaji wa Mazingira kwa kupiga picha ya Mazingira safi yanayomzunguka na kuwasilisha NEMC Kwa ajili ya mashindano hayo.

Maadhimisho hayo yalipambwa na mabalozi wa Mazingira pamoja na watumbuizaji nguli akiwemo Mrisho Mpoto pamoja na Mr. Tree na kuhudhuriwa na Viongozi mbalimbali akiwemo Mwenyekiti wa Bodi ya NEMC, Menejimenti ya NEMC, TANTRADE, STAMICO, Wanawake na Samia, Shirika la PUMA pamoja na wananchi waliotembelea maonesho ya sabasaba.



Ugawaji wa Zawadi kwa Wadau wengine 


Hakuna maoni:

Chapisha Maoni

NEMC YASHIRIKI MKUTANO WA SABA WA UMOJA WA MATAIFA KUHUSU MAZINGIRA

Baraza la Taifa la Hifadhi na Usimamizi wa Mazingira (NEMC) linashiriki Mkutano wa Saba (07) wa Umoja wa Mataifa kuhusu Mazingira (07th Unit...