Nyumbani

NEMC YASHIRIKI MKUTANO WA KAMATI YA KIMATAIFA GENEVA

Baraza la Taifa la Hifadhi na Usimamizi wa Mazingira NEMC limeshiriki Mkutano wa kamati ya kimataifa ya majadiliano ya kuanzisha mkataba wa kimataifa wa kukabiliana na uchafuzi unaotokana na Plastiki nchini nchini Uswisi mjini Geneva

Mkutano huo umehusisha jopo la wadau wa Mazingira kutoka nchini Tanzania likiongozwa Naibu Katibu Mkuu, Ofisi ya Makamu wa Rais (Mazingira) profesa Peter Msofe, Balozi wa Tanzania nchini Kenya, maafisa kutoka Ofisi ya Makamu wa Rais, NEMC, TBS, na GCLA ambao walishiriki kikamilifu kwa siku zote kumi za majadiliano ya kuanzishwa Mkataba huo.

Meneja wa Uzingatiaji wa Sheria (NEMC) Bw. Hamadi Taimuru akiwasilisha mada katika Mkutano huo

Naibu Katibu Mkuu Ofisi ya Makamu wa Rais (Mazingira) Profesa Peter Msoffe (wa kwanza kulia) na Bw. Hamadi Taimuru (wa pili kushoto) wakifuatilia Mkutano huo


Hata hivyo kutokana na mitazamo na misimamo ya nchi mbalimbali kulingana na maslahi ya nchi zao, majadiliano hayo hayakuweza kufikia muafaka na hivyo mwenyekiti wa Mkutano ndugu Luisaliaghirisha majadiliano mpaka pale atakapotangaza tarehe mpya ya kuendeleza majadiliano hayo na hatimaye kupata mkataba husika.

Majadiliano ya washiriki wa Mkutano huo ikiwa ni sehemu ya Mkutano huo

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni

NEMC YASHIRIKI MKUTANO WA SABA WA UMOJA WA MATAIFA KUHUSU MAZINGIRA

Baraza la Taifa la Hifadhi na Usimamizi wa Mazingira (NEMC) linashiriki Mkutano wa Saba (07) wa Umoja wa Mataifa kuhusu Mazingira (07th Unit...