Meneja wa Tafiti za Mazingira (NEMC) Dkt. Rose Sallema akizungumza wakati wa kikao kazi hicho
Baraza la Taifa la Hifadhi na Usimamizi wa Mazingira (NEMC) kwa kushirikiana na Shirika la Kimataifa la Uhifadhi wa Mazingira (IUCN) limefanya kikao kazi kujadili namna bora ya kukabiliana na tatizo la uchafuzi unaotokana na taka za plastiki katika ukanda wa bahari. Kikao hicho kimekusudia kuweka mikakati endelevu ya kudhibiti matumizi na utupaji holela wa plastiki, pamoja na kuhamasisha jamii kuhusu umuhimu wa kuhifadhi mazingira ya baharini kwa manufaa ya viumbe vya majini na ustawi wa binadamu kwa ujumla.
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni