Nyumbani

NEMC YAWANOA MAAFISA FORODHA KIGOMA - ELIMU YA USIMAMIZI WA MAZINGIRA

Baraza la Taifa la Hifadhi na Usimamizi wa Mazingira (NEMC) limeendelea kutoa mafunzo kwa Maafisa Forodha katika kituo cha mpakani cha Kigoma, ikiwa ni sehemu ya mwendelezo wa programu ya kujenga uelewa kuhusu usimamizi wa bidhaa hatarishi kwa mazingira zinazovuka mipaka.


Akifungua mafunzo hayo Oktoba 20, 2025 katika ofisi za Mamlaka ya Bandari Tanzania (TPA), Meneja wa Bandari Kigoma Bw. Edward Mabula amesisitiza umuhimu wa ushirikiano wa taasisi mbalimbali katika kulinda mazingira na kudhibiti uingizwaji wa bidhaa zisizo rafiki kwa mazingira.

“Ushirikiano baina ya taasisi kama NEMC, TRA, TPA, TBS, TMDA na wadau wengine ni muhimu sana katika kuhakikisha bidhaa zinazoingia nchini haziwezi kuathiri mazingira yetu,” amesema Bw. Mabula.


Kwa upande wa wawakilishi kutoka NEMC, wameeleza kuwa mafunzo hayo ni sehemu ya utekelezaji wa majukumu ya Baraza katika kusimamia utekelezaji wa Sheria ya Usimamizi wa Mazingira, Sura ya 191.

Aidha, wamefafanua kuwa lengo la mafunzo hayo ni kuwajengea uwezo Maafisa Forodha ili waweze kutambua mapema bidhaa hatarishi na kuchukua hatua stahiki kwa mujibu wa Sheria.

Mafunzo hayo ni mwendelezo wa programu inayoendeshwa na NEMC katika vituo vya mipakani vya Mtukula, Rusumo, Kigoma na Tunduma, ikilenga kuhakikisha bidhaa zote zinazoingia au kutoka nchini zinakidhi matakwa ya Sheria ya Usimamizi wa Mazingira.

Washiriki wa mafunzo ya Usimamizi wa Bidhaa hatarishi mipakani wakiwa katika picha ya pamoja mara baada ya mafunzo hayo





Hakuna maoni:

Chapisha Maoni

NEMC YASHIRIKI MKUTANO WA SABA WA UMOJA WA MATAIFA KUHUSU MAZINGIRA

Baraza la Taifa la Hifadhi na Usimamizi wa Mazingira (NEMC) linashiriki Mkutano wa Saba (07) wa Umoja wa Mataifa kuhusu Mazingira (07th Unit...