Baraza la Taifa la Hifadhi na Usimamizi wa Mazingira (NEMC) limeendelea kutoa mafunzo kwa Maafisa Forodha katika kituo cha mpakani cha Kigoma, ikiwa ni sehemu ya mwendelezo wa programu ya kujenga uelewa kuhusu usimamizi wa bidhaa hatarishi kwa mazingira zinazovuka mipaka.
Akifungua mafunzo hayo Oktoba 20, 2025 katika ofisi za Mamlaka ya Bandari Tanzania (TPA), Meneja wa Bandari Kigoma Bw. Edward Mabula amesisitiza umuhimu wa ushirikiano wa taasisi mbalimbali katika kulinda mazingira na kudhibiti uingizwaji wa bidhaa zisizo rafiki kwa mazingira.
“Ushirikiano baina ya taasisi kama NEMC, TRA, TPA, TBS, TMDA na wadau wengine ni muhimu sana katika kuhakikisha bidhaa zinazoingia nchini haziwezi kuathiri mazingira yetu,” amesema Bw. Mabula.
Aidha, wamefafanua kuwa lengo la mafunzo hayo ni kuwajengea uwezo Maafisa Forodha ili waweze kutambua mapema bidhaa hatarishi na kuchukua hatua stahiki kwa mujibu wa Sheria.
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni