Baraza la Taifa la Hifadhi na Usimamizi wa Mazingira (NEMC) kupitia Kanda ya Ilala limeendesha kikao cha masikilizano na wadau wa mazingira tarehe 21 Januari, 2026 katika Ukumbi wa Uhasibu, Ofisi za NEMC Mikocheni jijini Dar es Salaam, kwa lengo la kusikiliza na kushughulikia malalamiko ya mazingira kutoka kwa jamii zinazozunguka Kanda hiyo pamoja na kujenga uelewa wa pamoja kuhusu masuala ya mazingira na utekelezaji wa Sheria ya Usimamizi wa Mazingira.
Katika kikao hicho, NEMC ilisisitiza umuhimu wa ushirikiano kati ya jamii na wadau wa mazingira katika kulinda na kusimamia mazingira, kuhimiza wananchi kuzingatia sheria, taratibu na kanuni za mazingira, na kuahidi kuendelea kutoa elimu ya mazingira pamoja na kuchukua hatua stahiki kwa mujibu wa sheria ili kuhakikisha mazingira yanahifadhiwa kwa maendeleo endelevu na ustawi wa kizazi cha sasa na kijacho.
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni