Baraza la Taifa la Hifadhi na Usimamizi wa Mazingira NEMC limeshiriki mkutano wa siku mbili ulioandaliwa na Ofisi ya Makamu wa Rais wenye lengo la kuleta ushirikiano kuhusu masuala ya uhifadhi na usimamizi wa Mazingira baina ya Tanzania Bara na Zanzibar.
Mkutano huo umeanza Februari 16 , 2026 kwa ngazi ya wataalamu na 17 Februari, 2026 kwa ngazi ya viongozi Kisiwani Zanzibar.
Itakumbukwa kuwa, Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar zimeweka utaratibu wa wizara, Idara na Taasisi zisizo za Muungano za SJMT na SMZ zinazoshabihiana kimajukumu kufanya vikao vya kuimarisha ushirikiano ili kubadilishana uzoefu, kuimarisha ushirikiano wa kiutendaji na kujadili na kushughulikia changamoto mbalimbali za kiutendaji zilizopo baina ya pande hizo mbili
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni