Nyumbani

𝗡𝗘𝗠𝗖 𝗬𝗔𝗙𝗨𝗡𝗚𝗜𝗔 𝗨𝗝𝗘𝗡𝗭𝗜 𝗪𝗔 𝗠𝗔𝗝𝗘𝗡𝗚𝗢 𝗠𝗔𝗪𝗜𝗟𝗜 𝗠𝗜𝗞𝗢𝗖𝗛𝗘𝗡𝗜

Baraza la Taifa la Hifadhi na Usimamizi wa Mazingira (NEMC) limefungia ujenzi wa majengo mawili yaliyokuwa yanaendelea kujengwa katika eneo la Mikocheni, mtaa wa Regent, mkoani Dar es Salaam, kufuatia ukiukwaji wa taratibu za usimamizi wa mazingira. Majengo yaliyosimamishwa ni pamoja na VIENNATANZANIA CO LTD na TAFBROS LIMITED

Hatua hiyo imechukuliwa baada ya kubainika kuwa miradi hiyo ilikuwa inaendelea kuwa na vibali vya Tathmini ya Athari kwa Mazingira (EIA). NEMC imeagiza kusimamishwa mara moja kwa shughuli zote za ujenzi hadi taratibu zote za kisheria zitakapokamilika.

Hata hivyo NEMC imetoa angalizo kwa niradi yote inayoendelezwa bila kufata taratibu za Mazingira kusitisha na kufika ofisi za NEMC kwaajili ya kuanza mchakato wa Uzingatiaji wa Sheria kabla ya kukaguliwa na kupewa adhabu.





Hakuna maoni:

Chapisha Maoni

TIMU YA UKAGUZI WA MAZINGIRA KUTOKA NEMC MAKAO MAKUU NA KANDA YA ZIWA VICTORIA MASHARIKI WAADHIMISHA MEIMOSI 2026 KWA KUPANDA MITI MAKUMBUSHO YA MWL. JULIUS K. NYERERE, BUTIAMA

Timu ya watumishi wa Baraza la Taifa la Hifadhi na Usimamizi wa Mazingira (NEMC) wanaofanya ukaguzi wa mazingira katika mikoa ya Kanda ya Zi...