Nyumbani

NEMC NA THPS WAJADILI USHIRIKIANO KATIKA MASUALA YA AFYA YA JAMII YA MAZINGIRA

Baraza la Taifa la Hifadhi na Usimamizi wa Mazingira (NEMC) na Taasisi ya Tanzania Health Promotion Support (THPS) wamefanya kikao cha pamoja kuhusu ushirikiano katika masuala ya usimamizi wa mazingira na afya ya jamii tarehe 10 Machi 2026 katika Ukumbi wa Mikutano wa Baraza jijini Dar es Salaam. 

Katika kikao hicho, pande zote mbili zimejadiliana na kukubaliana kushirikiana katika kujengea wadau uelewa kuhusu afya ya binadamu na mazingira, kukabiliana na changamoto za mabadiliko ya tabianchi, kuimarisha tafiti kuhusu uhusiano kati ya mazingira na afya ya binadamu, pamoja na kuboresha usimamizi endelevu wa taka zitokanazo na huduma za afya.

Ushirikiano huu unalenga kuunga mkono juhudi za Taifa katika kulinda mazingira, kuboresha afya ya jamii na kuchochea maendeleo endelevu sambamba na utekelezaji wa Dira ya Taifa ya Maendeleo 2050, inayosisitiza umuhimu wa mazingira salama na jamii yenye afya kwa maendeleo ya kiuchumi na kijamii nchini.

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni

TIMU YA UKAGUZI WA MAZINGIRA KUTOKA NEMC MAKAO MAKUU NA KANDA YA ZIWA VICTORIA MASHARIKI WAADHIMISHA MEIMOSI 2026 KWA KUPANDA MITI MAKUMBUSHO YA MWL. JULIUS K. NYERERE, BUTIAMA

Timu ya watumishi wa Baraza la Taifa la Hifadhi na Usimamizi wa Mazingira (NEMC) wanaofanya ukaguzi wa mazingira katika mikoa ya Kanda ya Zi...